INUKA UANGAZE
 |
| Pastor Frank Andrew, Ufufuo na Uzima. |
Ninyi(mliookoka) ni nuru ya ulimwengu. Mathayo 5:14-16. Nuru hiyo
mliipata kutoka kwa Bwana Yesu imeandikwa1 John 1:4 'ndani yake ndimo
ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikua nuru ya watu' Sema Amen!
Kama
umeshampokea Yesu ndani yako kuna uzima ambao ndio nuru ing'aayo sana!
Kila siku unapokuja ktk bonde la kukata maneno unapoke maarifa ya rohoni
ambayo ndio ile nuru ile ukirudi nyumbani/kazini/shuleni...nuru
iliyoipokea ikang'ae kwa jina la Yesu!
Kitabu cha Mathayo 5:14-16
Bwana Yesu anasema kazi ya nuru ni kuangaza! Nuru iliyofichwa uvunguni
haina faida yoyote, lakini nuru ikiinuliwa juu itawaangaza wote waliomo
nyumbani.
Ndugu zangu dunia imejaa giza; mambo ambayo wanadamu
wamekosa majibu, magonjwa yasiyotibika, matukio ya kichawi ambayo
serikali hazina majibu yake....kila mahali kumejaa sintofahamu za kila
namna..giza limeifunika dunia.
Isaya 60: 1-3 " Ondoka uangaze; kwa maana nuru yako imekuja, na utukufu wa Bwana umekuzukia."
JINSI YA KUINUKA NA KUNG'AA
Kabla
nuru haijang'aa gizani hatua ya kwanza ni KUINUKA. Sema kuinuka! Isaya
60:1 imeanza na neno (Ondoka). Kuinuka maana yake ni kutengeneza msimamo
sawasawa na neno la Mungu. Kwa mfano wewe ni mgonjwa. Ukijua tu
imeandikwa 'kwa kupigwa kwake mliponywa' anza kutengeneza msimamo kwamba
sitakufa bali nitaishi, tengeneza msimamo kwa kupigwa kwake niliponywa!
Msimamo wako ukikaa sawa sawa na neno la Mungu ujue umeshainuka tayari.
Ujue umeshaipata nuru.
Hatua ya pili ni kung'aa. Imeandikwa Yohn 1:5
'nayo nuru yang'aa gizani wala giza halikuiweza. Ukishatengeneza
msimamo sawasawa na neno la Mungu anza kupiga majeshi...imeandikwa
sitakufa bali nitaishi...nakataa kufa kwa jina la Yesu, mauti nakufunga,
nakusambaratisha kwa damu ya mwanakondoo.....imeandikwa mabaya
hayatanipata mimi wala tauni hatakaribia hema yangu.....najitenga na
mabaya yote kwa jina la Yesu.....imeandikwa ndani yake tunaishi,
tunakwenda na kuwa na uhai wetu....mimi nitaishi kwa jina la
Yesu.Imeandikwa mkaribieni Mungu, mpingeni shetani nae
atawakimbia.....imeandikwa hulituma neno huwaponya! ...kulingana na giza
lililofunika maisha yako/njia yako/ mazingira yako ya wakati huo.
MIFANO YA WALIOANGAZA
1. I samwel 17: 17--
Goliati
alipoinuka kambia yote ya Isrel ilijaa giza(hawakujua cha kufanya hofu
kuu iliwafunika) alipokuja Daudi akatengeneza msimamo akainuka akampiga
Goliati nuru yake ikang'aa mbele ya majeshi yote ya Israel
2. 2wafalme 7: 3---
Isrel
ilikua kwny njaa, wamehusuriwa na adui.pande zote hawajui cha kufanya
(giza). Wakoma kumi wakapata nuru/ maarifa wakatengeneza msimamo
kulifuata jeshi ya washami kishindo chao kikawa kama radi wakang'aa kwa
ushindi mkuu kwa jina la Yesu!
BARAKA BAADA YA KUINUKA KUANGAZA
Isaya 60:4-22
- utajiri wa mataifa utakuwasilia
-wote watakuja kutoka sheba wataleta dhahabu na uvumba
-kondoo waume wa Nebayothi watakutumikia
-wageni watajenga kuta zako
-kila taifa na ufalme wa watu wasiotaka kukutumikia wataangamia
-utakua fahari ya milele
........and so much more
Toa Maoni Hapa Chini