Rais Kikwete atoa Shuhuda juu ya Askofu Kulola | Apostle Darmacy Blog MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 | Apostle Darmacy Blog

APOSTLE DAMAS

Breaking News

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, February 23, 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 

 

Goo

 

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 
About Muses Radio Player...
Version 2.1 (html5)

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.
-->

Tangaza nasi

Breaking News
Loading...

Soma App

Soma App
DOWNLOAD Somaapp NOW!

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Wednesday, September 4, 2013

Rais Kikwete atoa Shuhuda juu ya Askofu Kulola



Rais Kikwete aongoza mazishi ya Askofu Kulola
Na Apostle Darmacy Damas AnthonyRais Jakaya Kikwete akitoa salamu za rambiwambi.


Waziri Mkuu aliyejiuzulu ambaye pia ni Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa akisalimiana na Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Wilbroad Slaa jana wakati wa ibada ya mazishi ya Askofu Mkuu, Moses Kulola wa Kanisa la Evangelist Assemblies of God Tanzania (EAGT) aliyezikwa nje ya Kanisa la Calvary Bugando jijini Mwanza. 


 Rais Jakaya Kikwete ameongoza maelfu ya waombolezaji kumzika aliyekuwa Askofu Mkuu Moses Kulola wa Kanisa la Evangelist Assemblies of God Tanzania (EAGT). Kiongozi huyo alizikwa jana nje ya Kanisa la Calvary Bugando. 
Licha ya kuongoza mazishi hayo, Rais Kikwete pia alitoa ushuhuda kwamba licha ya kuwa muumini wa dini ya Kiislamu, Askofu Kulola wakati wa uhai wake mara kadhaa alikwenda Ikulu kumfanyia maombi.


Rais Kikwete katika salamu zake za rambirambi, alisema amekwenda kushiriki msiba huo kuungana na waombolezaji kutokana na kumfahamu Askofu Kulola ambaye alikuwa mtu wa watu.


“Tuzidi kuwaombea kwa Mungu, familia katika kipindi hiki kigumu, kwa jinsi nilivyomfahamu marehemu alikuwa mpenda watu, hakujali kabila wala hali zao, alijali utu na heshima hii ndiyo sababu na mimi alikuwa rafiki yangu,” alieleza Rais Kikwete.


Alibainisha kwamba licha ya kuwa Muislamu mara kadhaa Askofu huyo alifika kumwombea Ikulu na katika maombezi yake alisisitiza kuwa alikuwa akiwaombea Watanzania na nchi nzima kwa ujumla, hivyo aliwahimiza walio hai kumuenzi Askofu kwa vitendo.
hali ya simanzi na majonzi ilitawala katika mazishi hayo ambapo pia Rais Kikwete alimuelezea Dr.Moses Kulola kama mtu aliyefahamiana nae mda mrefu na mtu ambaye aliwahi pia kwenda ikulu na kumuombea na pia  kuiombea nchi ya Tanzania idumu katika Amani na mshikamano


aidha Rais Kikwete alimuelezea Dr.Moses Kulola kama mtu ambaye alikua mkweli mpenda watu watu na mtu ambaye hakua na ubaguzi wa kabila,dini rangi wala dhehebu na ndio maana hata leo hii watu wa madhehebu yote wamehudhuria hata katika mazishi yake.
"Mimi sio msukuma wala mimi sio mkristu lakini kikubwa kilichonifanya nifike katika mazishi ya ndugu yetu na mpendwa wetu huyu askofu  mkuu Dr.Moses Kulola ni vile maisha yake aliyoishi hapa duniani ambayo ni mahubiri tosha 
aliisimamia kweli bila kuogopa wala kutetereka ,,,,,penye baya alisema hili ni baya na penye zuri alisema hili ni zuri....kama asingekua mtu wa namna hiyo wala asingekua rafiki yangu...
 
 kuna kipindi alishakuja yeye pamoja na mama mpaka kwangu ikulu akanambia nimekuja nataka nikuombee wewe binafsi na pia niiombee nchi ya Tanzania kupitia wewe Raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ufanikiwe na upate kuongoza vema usiogope Mungu yupo pamoja nawe.
kwa namna mtu huyu maisha yake alivyoishi binafsi nimehuzunishwa sana baada ya kusikia kifo chake kwani taifa limepoteza mtu wa muhimu sana mtu aliyekua kila kukicha akiiombea tanzania iwe na amani na mshkamano na ndio maana leo hii wote tupo hapa bila kujali vyama vyetu wanasiasa dini zetu wala kabila zetu....kikubwa tumuenzi kwa kutenda yale aliyotufundisha.
alisema Rais Jakaya Kikwete


Kwa upande wake, Makamu Askofu Mkuu wa EAGT Asumwisye Mwaisabila, akizungumzia msiba huo kuwa marehemu Kulola alikuwa mchungaji wa aina yake na hivyo kuwataka wanaotaka kufanana naye kuomba kwa Mungu awajalie hekima.


“Alikuwa askofu wa ajabu sana, hata kama ungeweza kumtandikia mkeka ili alale, angelala. Jambo hili ni tofauti sana na maaskofu wa kileo ambao ukiwatendea hivyo watanung’unika na kukusema kila siku,” alieleza na kusisitiza wanapaswa kumuenzi kwa vitendo.



Katika Ibada ya maziko ya Askofu Kulola iliyoongozwa na Makamu Askofu Mkuu, Asumwisye Mwaisabila, mbali na Rais Kikwete pia Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibroad Slaa, aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Anthony Diallo, Wabunge William Ngeleja (Sengerema), Ezekiel Wenje (Nyamagana), Highness Kiwia (Ilemela) pamoja na Mchungaji Peter Msigwa, ambaye pia ni Mbunge wa Iringa Mjini.
Florah Mbasha na wajukuu wenzake wakiimba kwa huzuni.
Mchungaji Abiudi Misholi akiimba wimbo aliotunga takriban nusu saa mara baada ya kupata taarifa za msiba wa Askofu Kulola.

Nyota imezimika, anaimba mchungaji Abiudi Misholi


Wakati huohuo Rais Kikwete jana alisafiri kwenda Kampala, Uganda, kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi za Ukanda wa Maziwa Makuu.


Sehemu ya wageni waliohudhuria, Askofu Bruno Mwakibolwa wa EAGT Mito ya Baraka akiratibu baadhi ya mambo kwa simu.
                                                                                                       
Mashada


Askofu wa BCIC, Sylvester Gamanywa akiweka shada la maua kwenye kaburi la Askofu Moses Kulola.
Waziri mkuu aliyepita, Edward Lowasa akiweka shada la maua kwenye kaburi la Askofu Moses Kulola


Makamu Askofu MKuu wa EAGT, Mwaisabila akiweka shada la maua kuhitimisha zoezi, kisha mafundi wakachukua nafasi yao.
                         
Picha na matukio yote yaliyojiri katika mazishi ya shujaa wa injili Askofu Dr.Moses Kulola ni kama zinavyoonekana hapa chini
Rais Jakaya Kikwete akiwasili katika eneo ilipofanyika ibada ya mazishi ya askofu Moses Kulola
mama mjane akiweka udongo kwenye kaburi la mumewe Askofu Moses Kulola
 Mke wa Shujaa wa Injili akiweka Shada ya Maua
 
 


 


Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.