Wajibu wa kanisa kwa waongofu wapya hususani watu maarufu (Celebrities)
“Enendeni ulimwenguni kote mkaihubiri injili kwa kila kiumbe……….”
Mathayo 28;19
Kanisa la leo yaani jamii ya watu waliookoka ni wazi
kuwa mkazo mkubwa ni watu kuokoka kuliko namna ya kuwawezesha waongofu
hao wapya wadumu katika wokovu . Sio jambo la kushangaza kuona nguvu
inayotumika ili kuwafikia watu kuanzia mafungu ya fedha kwa ajili ya
uinjilisti na umishieni, Muda Maombi kwa ajili ya kuhubiri injili,
havifikii hata nusu ya nguvu inayotumika katika kuwajenga kiroho watu
ambao wamekata shauri katika harakati hizo za kumtangaza Kristo.
     |
Kristo ndiye mchungaji Mwema naye hatoacha kondoo wake hata mmoja apotee bali humfuatilia hadi ampate |
WATU MAARUFU (CEREBRITIES) NA WOKOVU
Inapotokea
watu maarufu Cebrities wakaamua kumpokea Kristo jamii ya watu
waliookoka hufurahi pasipo kujiuliza nini wajibu wao katika kuhakikisha
Cebrities hao wanadumu katika wokovu. Tumeshuhudia Cerebrities wengi
Duniani na Afrika mashariki wakiokoka na wengi wamedumu katika wokovu na
wengne wameshindwa kuendelea na wokovu.
Wajibu wakanisa kwa waongofu wapya wakiwemo ma Celebrities ni kuwaombea siku zote wasimame katika wokovu pasipo kukata tamaa Luka 18:1
Ifuatayo ni orodha ya watu maarufu hapa nchini na nchini Kenya waliokata shauri na kutangaza kuwa wameokoka.Wapo ambao wanaendelea na wokovu lakini pia wapo ambao kwa namna Fulani wamekwama njiani.
Joseph Kelvin Mapunda Q-Jay
 |
Joseph Mapunda Q jay
|
Kijana
huyu alikuwa mmoja wa wanamuziki wa kundi la Wakali Kwanza.
Alilipotiwa kumpokea Kristo januari mwaka huu. Q – JAY ni mchanga
katika wokovu na wengi wanamuona kama anajaribisha maisha ya Wokovu.
Changamoto
iliyopo ni kuwa ikiwa watu wengine wanamuona ni kama anajaribu, je
kanisa linamchukuliaje? Na kumsaidia vipi katika safari yake ya wokovu.
Q
Jay baada ya kuokoka alisema hatoingia studio na kuimba nyimbo za
injili mpaka baada ya miezi sita kwa sasa ameoa na anendelea na wokovu.
Jacob Stephen JB
 |
Jacob Stephen JB |
Huyu
ni mcheza Filamu maarufu hapa nchini na ni mmoja ya watu waliotangaza
kuwa wameokoka miaka kadhaa iliyopita na mpaka sasa anaendelea na
wokovu, JB anasali Mikocheni B Assemblies of GOD kanisa lililo chini ya
Mch Mama Getrude Rwakatare.
James Temu (Jimmy)
Huyu
Brother ni Muigizaji wa Filamu hapa nchini na pia Jimmy ni mtangazaji
wa Praise Power Radio. Ameshiriki katika movie nyingi. Jimmy Ameokoka
na anasali katika kanisa la Mtume Kingu lililoko jijini Dar es salaam.
Ni mmoja kati ya waigizaji wa Filamu ambao wameokoka na wako serious
kwenye wokovu.
 |
Uncle Jimmy
|
Emmanuel Mgaya (Masanja Mkandamizaji)
 |
Masanja Mkandamizaji akisikiliza Neno la Mungu katika Semina ya Mwl Mwakasege viwanja vya Biafra jijini Dar es salaam
|
Huyu
jamaa ni KWELI ameokoka na ni mmoja wa maceleb ambao wamemaanisha
katika wokovu. Yapata takribani mwaka sasa toka masanja aamue kumpokea
Kristo na amekuwa akizunguka sehemu mbalimbali huku akihubiri Neno la
Mungu.
Licha ya kuhubiri pia anayo album yake inayoitwa
Hakuna jipya na alishiriki kuimba mara kadhaa katika mkutano wa Askofu
Moses Kulola uliomalizika hivi karibuni katika viwanja vya jangwani
jijini Dar es salaam
Kwa
sasa Masanja anasali katika kanisa la EAGT Mito ya Baraka lililoko
Jangwani jijini Dar es salaam chini ya Askofu Bruno Mwakiborwa. Tofauti
na mastaa wengine Masanja toka aokoke hajawai kupata kashfa yeyote juu
ya wokovu wake.
Godwin Gondwe. Double G
 |
Double G |
Kati
Ya Watu waliodumu Katika Wokovu na Kukuwa basi ni Double G ambaye
amekuwa Mtangazaji wa Redio One na ITV, ambaye pia ni Lecturer katika
Chuo Cha Tumaini amekuwa kati ya ma-staa wa kuigwa, Double G yeye ni
Mshirika wa CCC.
KUTOKA KENYA
DNA Banjuka
 |
DNA |
Kijana
huyu kutoka nchini Kenya alifahamika sana Afrika Mashariki na Kati
baada ya kutoa nyimbo yake iitwayo BANJUKA. Mwaka mmoja baada ya kutoa
album yake ikiwa na nyimbo yake hiyo aliamua kumpokea Kristo kama Bwana
na Mwokozi wa maisha yake.
Katika
Interview mbalimbali DNA haachi kusema wakati wote huo kabla hajaokoka
alikuwa mlevi kupindukia.Kwa sasa huu ni mwaka wa pili DNA akiendelea
na wokovu. Kwa sasa licha ya kuimba nyimbo za Injili DNA ni mtangazaji
wa kituo kimoja cha Redio ya Kikristo jijini Nairobi.
Ummy Wenceslaus (DOKII)
 |
Ummy - Dokii |
Huyu
ni msanii mkongwe wa maigizo hapa nchini, kabla hajatangaza kuwa
ameokoka baada ya kuugua kwa muda mrefu alikuwa Muislamu. Baada ya
kuokoka na kuanza kusali kanisa la Universal lililoko maeneo ya mnazi
mmoja jijini Dar es salaam, Dokii aliwahi kutoa album ya nyimbo za
injili na alifanikiwa kuzunguka mikoani akiinadi album hiyo na
akitangaza matendo makuu ya Kristo Yesu.
Wengi
wamesema mengi juu ya wokovu wa Dokii, ila kilichonifanya nimuweke
hupa Dokii tofauti na wasanii wengine ni kauli zake juu ya wokovu.
Pamoja na yote anayopitia Dokii anakiri wazi kuwa ameokoka.
Celebrities’ wengine waliowahi kutangaza kuwa wameokoka wakiulizwa
swali hilo hupiga chenga.
Haijalishi
anapitia nini Maadam bado ndani yake anatamani kuendelea kusimama
zaidi, kanisa halina budi kumsemea positive na kumsaidia na sio kumpiga
vijembe eti ooh alidhani wokovu ni lele mama, mara hajafunga mkanda
Yuleee!, wengine ooh hakuhesabu gharama!. Lugha hizi kwa kanisa si
sahihi kwa kuwa changamoto anazokutana nazo Dokii na Celebrities wengine
ni kubwa hivyo anahitaji wapambanaji(kanisa) watakaoingia vitani
pamoja nae kwa utukufu wa Mungu.
MFANO WA KUIGA
Emmanuel Myamba
Katika
wasanii wa maigizo nchini huyu mtumishi ni mmoja kati wa watu
waliosimama kwenye wokovu. Ameokoka siku za nyuma wakati akiwa A Level
pale Jitegemee sekondari. Tofauti na wengine yeye aliokoka kabla hajawa
celebrity na ni mhitimu wa Chuo kikuu cha Dar es salaam alikochukua
masomo ya Sosholojia.
Myamba
kwa sasa anakampuni yake ya kutengeneza Filamu iitwayo Born again
Films. Mtumishi huyu ni mfano wa kuigwa kwa wasanii wa Filamu na maigizo
nchini. Ameweza kuonyesha kuwa unaeweza kuwa superstar wa Filamu na
usilewe sifa bali ukatumia Filamu katika kumtangaza Kristo, kwa sasa
anasali kanisa la Living Water Centre chini ya Apostle Ndegi.
Hitimisho
Kanisa
bado linawajibu wa kuwaombea na kuwafundisha waongofu wapya kwa
upendo, na tusitake mtu afundishwe kuendesha gari leo kisha kesho awe
dreva mzoefu, bali tuwape muda na kuwaelekeza kadri ambavyo Roho
anatusaidia kuwaelekeza kwa utukufu wa Mungu.
Kwa kuwa Kwa Neema ya Kristo atawawezesha kusimama, Efeso 3 :20
“Na atukuzwe yeye awezaye kutenda mambo ya ajabu mno kuliko yale
tuyaombayo au tuyawazayo” hivyo Kristo yupo kuwapa nguvu ya kuendelea
mbele na wokovu.
 |
Mwandishi wa apostledarmacy.blogspot.com
|
Habari hii ni kwa hisani ya apostledarmacy.blogspot.com
Toa Maoni Hapa Chini