WATU MAARUFU (CEREBRITIES) NA WOKOVU | Apostle Darmacy Blog MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 | Apostle Darmacy Blog

APOSTLE DAMAS

Breaking News

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, February 23, 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 

 

Goo

 

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 
About Muses Radio Player...
Version 2.1 (html5)

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.
-->

Tangaza nasi

Breaking News
Loading...

Soma App

Soma App
DOWNLOAD Somaapp NOW!

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Wednesday, December 4, 2013

WATU MAARUFU (CEREBRITIES) NA WOKOVU

Wajibu wa kanisa kwa waongofu wapya hususani watu maarufu (Celebrities) 

“Enendeni ulimwenguni kote mkaihubiri injili kwa kila kiumbe……….”

Mathayo 28;19

 Kanisa la leo yaani jamii ya watu waliookoka ni wazi kuwa mkazo mkubwa ni watu kuokoka kuliko namna ya kuwawezesha waongofu hao wapya wadumu katika wokovu . Sio jambo la kushangaza kuona nguvu  inayotumika ili kuwafikia watu kuanzia mafungu ya fedha kwa ajili ya uinjilisti na umishieni, Muda Maombi kwa ajili ya kuhubiri injili, havifikii hata nusu ya nguvu inayotumika katika kuwajenga kiroho watu ambao wamekata shauri katika harakati hizo za kumtangaza Kristo. 

Kristo ndiye mchungaji Mwema naye hatoacha kondoo wake hata mmoja apotee bali humfuatilia hadi ampate

 

WATU MAARUFU (CEREBRITIES) NA WOKOVU


Inapotokea watu maarufu Cebrities wakaamua kumpokea Kristo jamii ya watu waliookoka hufurahi pasipo kujiuliza nini wajibu wao katika kuhakikisha Cebrities hao wanadumu katika wokovu. Tumeshuhudia Cerebrities wengi Duniani na Afrika mashariki wakiokoka na wengi wamedumu katika wokovu na wengne wameshindwa kuendelea na wokovu.

Wajibu wakanisa kwa waongofu wapya wakiwemo ma Celebrities ni kuwaombea siku zote wasimame katika wokovu pasipo kukata tamaa Luka 18:1

Ifuatayo ni orodha ya watu maarufu hapa nchini na nchini Kenya waliokata shauri na kutangaza kuwa wameokoka.Wapo ambao wanaendelea na wokovu lakini pia wapo ambao kwa namna Fulani wamekwama njiani.

Joseph Kelvin Mapunda Q-Jay

Joseph Mapunda Q jay

Kijana huyu alikuwa mmoja wa wanamuziki wa kundi la Wakali Kwanza. Alilipotiwa kumpokea Kristo januari mwaka huu. Q – JAY ni mchanga katika wokovu na wengi wanamuona kama anajaribisha maisha ya Wokovu.


Changamoto iliyopo ni kuwa ikiwa watu wengine wanamuona ni kama anajaribu, je kanisa linamchukuliaje? Na kumsaidia vipi katika safari yake ya wokovu.

Q  Jay baada ya kuokoka alisema hatoingia studio na kuimba nyimbo za injili mpaka baada ya miezi sita kwa sasa ameoa na anendelea na wokovu. 
 
Jacob Stephen JB

Jacob Stephen JB
Huyu ni mcheza Filamu maarufu hapa nchini na ni mmoja ya watu waliotangaza kuwa wameokoka miaka kadhaa iliyopita na mpaka sasa anaendelea na wokovu,  JB anasali Mikocheni B Assemblies of GOD kanisa lililo chini ya Mch Mama Getrude Rwakatare.
 
 
 
James Temu (Jimmy)
Huyu Brother ni Muigizaji wa Filamu hapa nchini na pia Jimmy ni mtangazaji wa Praise Power Radio. Ameshiriki katika movie nyingi. Jimmy Ameokoka na anasali katika kanisa la Mtume Kingu lililoko jijini Dar es salaam. Ni mmoja kati ya waigizaji wa Filamu ambao wameokoka  na wako serious kwenye wokovu.

Uncle Jimmy

 
 
Emmanuel Mgaya (Masanja Mkandamizaji)

Masanja Mkandamizaji akisikiliza Neno la Mungu katika Semina ya Mwl Mwakasege viwanja vya Biafra jijini Dar es salaam

Huyu jamaa ni KWELI ameokoka na ni mmoja wa maceleb ambao wamemaanisha katika wokovu. Yapata takribani mwaka sasa toka masanja aamue kumpokea Kristo na amekuwa akizunguka sehemu mbalimbali huku akihubiri Neno la Mungu.

Licha ya kuhubiri pia anayo album yake inayoitwa Hakuna jipya na alishiriki kuimba mara kadhaa katika mkutano wa Askofu Moses Kulola uliomalizika hivi karibuni katika viwanja vya jangwani jijini Dar es salaam

Kwa sasa Masanja anasali katika kanisa la EAGT Mito ya Baraka lililoko Jangwani jijini Dar es salaam chini ya Askofu Bruno Mwakiborwa. Tofauti na mastaa wengine Masanja toka aokoke hajawai kupata kashfa yeyote juu ya wokovu wake.

Godwin Gondwe. Double G

Double G
 
 

Kati Ya Watu waliodumu Katika Wokovu na Kukuwa basi ni Double G ambaye amekuwa Mtangazaji wa Redio One na ITV, ambaye pia ni Lecturer katika Chuo Cha Tumaini amekuwa kati ya ma-staa wa kuigwa, Double G yeye ni Mshirika wa CCC.

 KUTOKA KENYA 

DNA Banjuka

DNA
Kijana huyu kutoka nchini Kenya alifahamika sana Afrika Mashariki na Kati baada ya kutoa nyimbo yake iitwayo BANJUKA. Mwaka mmoja baada ya kutoa album yake ikiwa na nyimbo yake hiyo aliamua kumpokea Kristo kama Bwana na Mwokozi wa maisha yake.

Katika Interview mbalimbali DNA haachi kusema wakati wote huo kabla hajaokoka alikuwa mlevi kupindukia.Kwa sasa huu ni mwaka wa pili DNA akiendelea na wokovu. Kwa sasa licha ya kuimba nyimbo za Injili DNA ni mtangazaji wa kituo kimoja cha Redio ya Kikristo jijini Nairobi.
 
 
 
 
 
Ummy Wenceslaus (DOKII)


Ummy - Dokii
Huyu ni msanii mkongwe wa maigizo hapa nchini, kabla hajatangaza kuwa ameokoka baada ya kuugua kwa muda mrefu alikuwa Muislamu. Baada ya kuokoka na kuanza kusali kanisa la Universal lililoko maeneo ya mnazi mmoja jijini Dar es salaam, Dokii aliwahi kutoa album ya nyimbo za injili na alifanikiwa kuzunguka mikoani akiinadi album hiyo na akitangaza matendo makuu ya Kristo Yesu.

Wengi wamesema mengi juu ya wokovu wa Dokii, ila kilichonifanya nimuweke hupa Dokii tofauti na wasanii wengine ni kauli zake juu ya wokovu. Pamoja na yote anayopitia Dokii anakiri wazi kuwa ameokoka. Celebrities’ wengine waliowahi kutangaza kuwa wameokoka wakiulizwa swali hilo hupiga chenga.


Haijalishi anapitia nini Maadam bado ndani yake anatamani kuendelea kusimama zaidi, kanisa halina budi kumsemea positive na kumsaidia na sio kumpiga vijembe eti ooh alidhani wokovu ni lele mama, mara hajafunga mkanda Yuleee!, wengine ooh hakuhesabu gharama!. Lugha hizi kwa kanisa si sahihi kwa kuwa changamoto anazokutana nazo Dokii na Celebrities wengine ni kubwa hivyo anahitaji wapambanaji(kanisa) watakaoingia vitani pamoja nae kwa utukufu wa Mungu.
 

MFANO WA KUIGA 


Emmanuel Myamba

Katika wasanii wa maigizo nchini huyu mtumishi ni mmoja kati wa watu waliosimama kwenye wokovu. Ameokoka siku za nyuma wakati akiwa A Level pale Jitegemee sekondari. Tofauti na wengine yeye aliokoka kabla hajawa celebrity na ni mhitimu wa Chuo kikuu cha Dar es salaam alikochukua masomo ya Sosholojia.

Myamba kwa sasa anakampuni yake ya kutengeneza Filamu iitwayo Born again Films. Mtumishi huyu ni mfano wa kuigwa kwa wasanii wa Filamu na maigizo nchini. Ameweza kuonyesha kuwa unaeweza kuwa superstar wa Filamu na usilewe sifa bali ukatumia Filamu katika kumtangaza Kristo, kwa sasa anasali kanisa la Living Water Centre chini ya Apostle Ndegi.
 

Hitimisho

Kanisa bado linawajibu wa kuwaombea na kuwafundisha waongofu wapya kwa upendo, na tusitake mtu afundishwe kuendesha gari leo kisha kesho awe dreva mzoefu, bali tuwape muda na kuwaelekeza kadri ambavyo Roho anatusaidia kuwaelekeza kwa utukufu wa Mungu.

Kwa kuwa Kwa Neema ya Kristo atawawezesha kusimama, Efeso 3 :20 “Na atukuzwe yeye awezaye kutenda mambo ya ajabu mno kuliko yale tuyaombayo au tuyawazayo” hivyo Kristo yupo kuwapa nguvu ya kuendelea mbele na wokovu.

 Mwandishi wa apostledarmacy.blogspot.com

Habari hii ni kwa hisani ya  apostledarmacy.blogspot.com

 

 

 



Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.