Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Mitihani
(Necta), Dk. Joyce Ndalichako, akitangaza matokeo ya mtihani wa taifa wa
kidato cha nne mbele ya waandishi wa habari jijini Dar es Salaa.
Matokeo
ya mtihani wa taifa wa kidato cha nne yaliyotangazwa jana yanaonyesha
kwamba wasichana wamewapiku kwa mbali wavulana, wakikalia nafasi nane
kati ya kumi bora, huku nusu ya watahiniwa wote wakiambulia daraja
sifuri.
Katika
matokeo ya mtihani huo yaliyotangazwa na Katibu Mtendaji wa Baraza la
Taifa la Mitihani (Necta), Dk Joyce Ndalichako, jumla ya watahiniwa
352,840 waliofanya mtihani huo ni 177,021 tu waliofaulu.
Matokeo
ya mtihani huo uliofanyika mwaka Oktoba mwaka jana pia yanaonyesha kuwa
watahiniwa wanne wamefutiwa matokeo kwa kuandika matusi mazito kwenye
karatasi za kujaza majibu.
Matokeo hayo yanaonyesha kuwa shule binafsi 10 ndizo zinazoongoza katika kundi la shule kumi bora kitaifa zilizofanya vizuri.
Dk.
Ndalichako alisema watahiniwa wa shule waliosajiliwa ni 363,589, lakini
waliofanya mitihani ni 352,840, waliofaulu wakiwa ni 177,021 sawa na
asilimia 50.4.
Katika kundi la waliofaulu, wasichana ni 69,996 sawa na asilimia 43.3 na wavulana ni 107,025 sawa na asilimia 56.
Alisema watahiniwa binafsi waliosajiliwa walikuwa 94,525 na kati ya hao waliofaulu walikuwa 46,064 sawa na asilimia 52.
Katika
ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliyopata watahiniwa wa shule,
Dk. Ndalichako alisema 40, 388 sawa na asilimia 11.5 wamefaulu katika
madaraja ya I hadi III na kwamba wasichana waliofaulu katika madaraja
hayo ni 12,583 na wavulana ni 27,805.
Alisema jumla ya wanafunzi waliopata daraja 0 ni 174,193 ambao ni karibu nusu ya wanafunzi wote waliofanya mitihani hiyo.
Jedwali
la matokeo linaonyesha kuwa wavulana waliopata darala la kwanza I ni
3,874 na wasichana ni 1,489, daraja la II wavulana ni 7,003 na wasichana
ni 2,939, daraja la III wavulana ni 16,928, wasichana ni 8,155 na
daraja la IV wavulana ni 79,220 na wasichana ni 57,413.
SHULE KALI 10
Alitaja
shule 10 zilizoongoza kitaifa na mikoa yake katika mabano kuwa ni
- Uru
Seminary (Kilimanjaro),
- St Francis Girls (Mbeya),
- Feza Boys (Dar es Salaam),
- St Mary Goreti (Kilimanjaro),
- St Joseph’s Sem
Iterarambogo (Kigoma) na
- Barbro-Johanson (Dar es Salaam).
WANAFUNZI WAKALI 10
Aliwataja
wanafunzi bora 10 kitaifa ambao walifanya vizuri kuliko wote na shule
zao katika mabano kuwa ni
- Lucylight Mallya na Maria-Dorin Shayo (Marian
Girls).
- Sherryen Cessar (Barbro-Johanson),
- Diana Abel Matabwa (St Francis
Girls),
- Neema Joey Kafwimi (St Francis) na
- Beatrice Issara (St Mary
Goreti)
- Johnston Dedani (Ilboru) mkoani Arusha,
- Samwel M. Emmanuel (Moshi
Tech),
- Bertha Sanga (Marian Girls) na
- Bernadetha Kalluvya (St Francis
Girls).
Aliwataja
wavulana kumi walioongoza kitaifa
- kuwa ni Johnston Dedani (Ilboru),
- Samwel Emmanuel (Moshi Tech),
- Jimoku Salum (Shinyanga Sekondari),
- Amaniel Barabara (Arusha Day),
- Aswile Mwambembe (Kibaha),
- James Mwitondi
(Loyola), Gasper Mung’ong’o (Loyola),
- Yohane Kihaga (Don Bosco Seminary
(Iringa) na
- Tonny Tarimo wa (Msolwa, Morogoro).
Dk.
Ndalichako alisema Necta inashikilia matokeo ya watahiniwa 1,448
waliofanya mitihani bila kulipa ada hadi hapo watakapolipa pamoja na
faini katika kipindi cha miaka miwili.
Alisema watahiniwa 311 wamefutiwa matokeo yao baada ya kubainika kuwa walifanya udanganyifu wa aina mbalimbali.
Katika
hatua nyingine, Dk. Ndalichako aliwaonya wanafunzi wa kidato cha sita
ambao wanatarajia kufanya mitihani yao mwezi ujao kuacha kuandika matusi
kwenye mitihani yao hata kama imewashinda.
“Nawaomba
kidato cha sita wasifanya mchezo huu kabisa, maana inaonekana kama
inaanza kuwa mazoea. Mwaka jana kulikuwa na mwanafunzi mmoja aliyeandika
matusi kwenye karatasi ya majibu mwaka huu idadi imeongezeka na kuwa
wanne,” alisema Dk. Ndalichako.
KUANGALIA
MATOKEO YA MITIHANI
Matokeo ya
Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) uliofanyika Novemba 2013 yanapatikana katika tovuti
http://41.188.155.122/CSEE2013/olevel.htm
Ni kwa hisani ya http://apostledarmacy.blogspot.com/
