KUNA FAIDA GANI YA KUWA NA MAOMBI YA MUDA MREFU? | Apostle Darmacy Blog MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 | Apostle Darmacy Blog

APOSTLE DAMAS

Breaking News

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, February 23, 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 

 

Goo

 

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 
About Muses Radio Player...
Version 2.1 (html5)

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.
-->

Tangaza nasi

Breaking News
Loading...

Soma App

Soma App
DOWNLOAD Somaapp NOW!

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Saturday, March 22, 2014

KUNA FAIDA GANI YA KUWA NA MAOMBI YA MUDA MREFU?


Zipo faida nyingi sana za kuwepo maombi ya muda mrefu kwa mtu anayetaka kuona MUNGU akimpigania katika mambo yake.



1)    Maombi haya yanatoa nguvu ya kutosha ambayo humfanya MUNGU atume malaika zake waje kushughulika na haja yako.                         
                      Efeso 3:20
                      Yakobo 5:16b, Matendo 12:5-11
                       Danieli 10:1-2,11-14.
Kutokana na utaratibu wa MUNGU wa kutenda kutokana na nguvu wanazoachilia watu wake basi ni muhimu kuwa watu waombe kwa muda mrefu ili wajenge nguvu ambayo MUNGU anapoitumia unakuja ushindi.

     = Namna nyingine za kuachilia nguvu za kiroho tofauti na maombi.
·       Kusoma sana NENO LA MUNGU.
Katika neno la Mungu unapata msaada na mwongozo wa kiimani ambao huo unakupa mbinu za kuishi maisha matakatifu. Unapoishi katika utakatifu ndipo unapojenga mazingira mazuri ya MUNGU kusikiliza maombi yako na kukuhudumia.
              1 Petro 3:12, Zaburi 16:3
              2 Nyakati 7:14-16.
    >Neno la Mungu hukupa nguvu ya kushinda majaribu,na unaposhinda jaribu kwa neno unakuwa tayari umeachilia nguvu ambayo MUNGU anaitumia kukufungulia baraka zingine. Mathayo 4:1-10.

·       Kutoa SADAKA
Hii ni moja ya njia muhimu sana katika kuachilia nguvu ya kiroho. Unapotoa sadaka unaigusa madhabahu ya MUNGU na kumfanya ashuke kukuhudumia.
             Malaki 3:10, Matendo 10:30-31.
Hapa Mungu anatusihi tumjaribu kwa sadaka ili afungue milango ya baraka kutumwagia; hiki ndicho alichofanya kornelio na Mungu akamkumbuka.

·       KUSIFU kwa hali ya juu na katika roho.
Mungu wetu ni Mungu anayependa kusifiwa, kwa hiyo unapotoa sifa kwake unauburudisha moyo wake na kumfanya ashuke kukuhudumia haja yako.
               Matendo 16:25-26

·        USHUHUDA wa matendo makuu ya Mungu.
Hapa unamwinua Mungu na kumuaibisha shetani hivyo MUNGU anatukuka na kukusaidia zaidi ili uendelee kumshuhudia na kumtukuza,
                Ufunuo 12:11a
 

2)     Maombi haya yanakupa nguvu ya kutosha kuweza kupambana na milango ya kuzimu.
                        1 Petro 5:8-9a
Kuna wakati unaweza kujiuliza ni kwa nini unaandamwa na roho chafu au nguvu za giza licha ya kwamba umeombea jambo hilo hata kwa muda mrefu. Unachoyakiwa kujua ni kwamba nguvu unayoachilia bado haijatosha kuyaangusha malango ya kuzimu yanayokuandama;hivyo inakupasa uombe zaidi hadi uone ushindi.
         Mtumishi mmoja alikuwa akishudia jinsi alivyoandamwa na roho ya uzinzi kwa muda mrefu, akasema niliomba sana lakini roho hiyo haikuniacha. Baada ya hapo nilifunga kwa muda wa mwezi mmoja lakini sikupata ushindi,ndipo nikaenda kuwashirikisha wanamaombi wenzangu na wakafunga siku tano, ndipo MUNGU akatoa maono kwamba ukoo wetu unaandamwa na uzinzi hivyo alikuwa amenipa mzigo mimi wa kuomba mpaka roho hiyo itakapoachia ukoo; alisema.
         Tunachojifunza hapa ni kwamba wakati mwingine hupati majibu ya maombi yako kwa sababu umebeba mzigo mkubwa ambao unahitaji nguvu kubwa kuutua,hivyo unapoona hali kama hizo omba msaada wa watu wengine wakusaidie kuachilia nguvu iletayo ushindi.


3)     Maombi haya humkumbusha MUNGU kuhusu hitaji lako ulilowahi kumwomba.
                    Isaya 62:6-7,1 Samweli1:10-12,20
                    Luka 1:5-20.
Kuna wakati unapoomba, unajibiwa lakini MUNGU anakuwa anasubiri kuiona juhudi yako katika kufuatilia maombi unayoomba. Kwa hiyo usipoomba mara kwa mara unakuta majibu yanachelewa kwa kutokukumbushia kwako.

4)      Maombi haya hukupa nguvu ya kuweza kushinda majaribu.
Kuna wakati watu hujiuliza ni kwa nini watumishi wa Mungu wanaanguka na kuacha wokovu? Suala ni kwamba unapookoka unatangaza vita na shetani hivyo kila wakati anakuwa anakuwinda akuangushe,na hivyo anatuma majeshi yake kukushambulia. Sasa unapokosa nguvu ya kutosha ndipo unakuta mtu anazidiwa na nguvu za ibilisi na hatimaye anaanguka.
         Hii ndio sababu iliyomfanya YESU awasisitize wanafunzi wake waombe ili wasiingie majaribuni, Mathayo 26:41.

5)     Maombi haya hukujengea mazingira ya kukaa katika utukufu wa MUNGU na kukuwezesha kukaa mbali na dhambi.
Unapokaa katika maombi kwa muda mrefu, moyo wako unakua unafunikwa na roho mtakatifu na hivyo muda wako mwingi utakuwa unamtafakari MUNGU na hii itakuweka mbali na kuzifikiria tamaa za ulimwengu huu.


6)     Maombi haya huubadilisha utu wa kale na kuleta utu ambao ni wa utukufu.
Mtu kabla hajaokoka anakuwa amefungwa kwenye roho mbalimbali chafu, anapookoka anasafishwa na kupewa utu upya lakini kuna roho nyingine unakuta zina maagano makubwa na hivyo suala tu la kuokoka haliziondoi roho hizo ndani ya mtu.
       Mtu huyu atahitajika kuomba kwa muda mrefu au watu wengine wamsaidie ili kuachilia nguvu ya kutosha itakayotumika kumfungua.
       Wakati tuko shule kuna binti mmoja tulimfanyia huduma, naye alikuwa anaandamwa na magonjwa ya kila mara tena yasioeleweka. tulipokuwa tunamwombea alikuwa anafunguliwa lakini baada ya siku chache tu alikuwa akirudia hali zilezile. Hatukukata tamaa na hatimaye MUNGU akasema kuwa kuna mambo elfu moja yaliokuwa yamemfunga na baada ya kuomba kwa miezi kama saba Mungu akasema limebakia jambo moja na iwapo tukilishinda hilo atakuwa huru kabisa.
       Sasa unaweza kuona jinsi ambavyo ni hatari kufanya maombi kwa ufupi.
      Kuna wengine wakati hawajaokoka walikuwa wazinzi au walevi, wanapookoka unakuta roho hizo bado zinawaandama, na wengine waanza kuona kuwa hawauwezi wokovu. suala ni kwamba watu hawa wanatakiwa waendelee kuomba zaidi ili MUNGU apate nguvu ya kutumia ili awafungue.


7)   Maombi haya hukupa amani ya kristo ambayo hukusaidia katika kufanya maamuzi sahihi juu ya mambo yako.
Kuna wakati watu hufanya maamuzi ambayo baadae huja wakayajutia, na wakati mwingine unaweza kukuta walimwomba MUNGU. Sasa tujiulize ni kwa nini wafanye uamuzi ambao baadae wanaujutia?.
         Jibu ni kwamba unakuta maombi aliyofanya mtu huyu hayatoi nguvu ya kutosha kumfanya MUNGU ashiriki kwenye maamuzi yako. Hiki ndicho kilimfanya YESU aombe usiku kucha alipotaka kuwachagua mitume na ndicho kiliwafanya mitume waombe walipotaka kuwaweka wakfu Barnaba na Sauli.
                     Luka 6:12-13, Matendo 12:3-4.

8)    Maombi haya yatakupa nafasi kubwa sana ya kusikilizwa mbele za Mungu.
Kuna mambo mengine MUNGU anakuwa hana mpango wa kuyafanya lakini unapozidisha kuliomba basi Mungu anaingia kazini kulishughulikia.
                     Yakobo 5:17-18.

NB: "Hakuna kipimo kamili cha muda ambao mtu anatakiwa kuutumia katika maombi kwa siku. Muda wa mtu kuomba utategemea msukumo wa roho mtakatifu ndani ya mwombaji, lakini pia ni vizuri ukawa na utaratibu kwamba mwisho wa maombi yako ni pale unapoona majibu ya maombi yako"

     
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.