LIVE UZINDUZI WA BOMA LA MAKUBUSHO YA MKOA WA IRINGA NA KITUO CHA UTAMADUNI | Apostle Darmacy Blog MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 | Apostle Darmacy Blog

APOSTLE DAMAS

Breaking News

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, February 23, 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 

 

Goo

 

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 
About Muses Radio Player...
Version 2.1 (html5)

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.
-->

Tangaza nasi

Breaking News
Loading...

Soma App

Soma App
DOWNLOAD Somaapp NOW!

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Saturday, June 25, 2016

LIVE UZINDUZI WA BOMA LA MAKUBUSHO YA MKOA WA IRINGA NA KITUO CHA UTAMADUNI


Uzinduzi wa Boma la Makumbusho ya Mkoa na Kituo cha Utamaduni

Ofisin ya mkuu wa mkoa wa Iringa Pamoja na Chuo kikuu cha Iringa siku ya tarehe 25/06/2016 kutakuwa  na uzinduzi wa Boma la Kihistoria  

 Kutakuwa na matukio mbalimbali yatakayoambatana na ufunguzi ikiwemo maonesho ya kitamaduni na sherehe rasmi za ufunguzi. Tunawakaribisha wakazi na watanzania wote kuja kusheherekea utamaduni na historia ya nyanda za juu kusini.

Pamoja na maonesho mbalimbali ya kuvutia ikiwemo Historia ya Iringa, Uganga na tiba asili, Hazina na asili ya Utamaduni wa Mkoa wa Iringa, pia kuna jambo la ziada la kujifunza kwa kila mtu.


Tafadhali jiunge nasi na kuona matokeo ya miaka kadhaa ya kazi ya kujitolea ya kulifufua Boma la iringa na kulifanya kuwa alama ya kipekee  kusini mwa Tanzania.


  

Hili ndilo jengo la makumbusho ambalo linaziduliwa leo.

  
Mgeni Rasmi ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Dk Augustine Mahiga.

MKUU wa Chuo Kikuu cha Iringa (IUCo), Profesa Joshua Madumulla amesema Nyumba ya Makumbusho ya Mkoa wa iringa itafanya kazi kubwa ya kukusanya na kutunza vitu mbalimbali vya kale.
MKUU wa Chuo Kikuu cha Iringa (IUCo), Profesa Joshua Madumulla

Vitu hivyo vya kisayansi, sanaa na historia vitatoa fursa kwa jamii ya ndani na nje ya nchi kujionea hazina ya urithi uliopo mkoani Iringa. Lina vitu mbali mbali vya zamani vya kihistoria vikiwemo
Mifupa ya Binadamu wa zamani
Vyungu
Pasi ya chuma
Historia  fupi ya mke  wa Mkwawa

“Uwekezaji katika urithi wa utamaduni hauna budi kupokelewa kama sehemu muhimu ya program itakayosaidia kukuza uchumi wa jamii husika na taifa kwa ujumla,”alisema.

Ukarabati wa nyumba hiyo iliyojengwa takribani miaka 116 iliyopita na utawala wa mjerumani aliyeitumia kama boma lake kuu, umefanywa kupitia mradi wa Kuendeleza Utamaduni Nyanda za Juu Kusini (Fahari Yetu) unaofadhiliwa na umoja wa nchi za Ulaya (EU) kwa zaidi ya Sh Milioni 230.

Jan Küver   Meneja wa fahari yetu

Project Manager at fahari yetu - Southern Highlands Culture Solutions

“Fursa ya kulibadili jengo hilo la boma la kihistoria kuwa jumba la makumbusho ni msingi imara wa kukataa hatari ya kuyumbishwa na mabadiliko yasiyoleta tija katika kukuza na kuendeleza tamaduni zetu na utalii wa kiutamaduni nchini,” alisema.

Meneja msaidizi wa mradi huo unaokishirikisha chuo hicho kikuu, Jimson Sanga alisema uzinduzi wa nyumba hiyo utafanywa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Dk Augustine Mahiga.
Meneja msaidizi wa mradi huo unaokishirikisha chuo hicho kikuu, Jimson Sanga

Sanga alisema  katika hafla hiyo itakayowashirikisha mawaziri wengine na viongozi mbalimbali wa serikali, siasa, mila, utamaduni na taasisi mbalimbali za ndani na nje ya nchi, utakwenda sambamba na maonesho ya rasilimali za utamaduni na historia ya mkoa wa Iringa.

Wizara ya Maliasili na Utalii imetoa kibali kwa Chuo Kikuu cha Iringa kulikarabati na kulihuisha jengo lililojengwa na wakoloni wa kijerumani miaka 114 iliyopita maarufu kama Iringa Boma na kuwa jumba la makumbusho.

Jengo hilo ambalo litafanyiwa ukarabati na mradi wa kuendeleza na kukuza utamaduni wa asili kanda ya Nyanda za Juu Kusini unaoitwa Fahari yetu unaotekelezwa na Chuo Kikuu cha Iringa kwa ufadhili wa Jumuiya ya nchi za Ulaya kwa zaidi ya miaka 50 iliyopita limekuwa likitumika kwa shughuli mbalimbali za Serikali ikiwemo ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Iringa.

Jengo hilo lililojengwa kwa usanifu wa hali juu kwa kutumia mawe, tofali zilizochomwa na tope au udongo na wakoloni wa kijerumani yapata miaka 114 iliyopita limekuwa Makao Makuu ya ofisi ya Mkuu wa wilaya ya Iringa kwa zaidi ya miaka 50 iliyopita.

Kutokana na kuwa na historia ya kuvutia, Serikali kupitia idara ya mambo kale imekuwa na mchakato wa kuligeuza kuwa jumba la makumbusho ambapo baada ya ofisi mpya ya Mkuu wa wilaya ya Iringa iliyogharimu zaidi ya shilingi bilioni 1.8 kukamilika.

Kwa mujibu wa Naibu Mkuu Chuo Kikuu cha Iringa Utawala Dokta Hosea Mpogole, chuo kikuu hicho kupitia mradi wake wa Fahari Yetu wamepata kibali cha kukarabati jengo hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari, Katibu Tawala wa Mkoa wa Iringa Wamoja Ayubu amesema lengo ni kulibadili jengo hilo na kulifanya kuwa jumba la makumbusho kwa kukusanya na kuweka ama kutunza kumbukumbu, kufanya maonesho mbalimbali ya urithi wa utamaduni wa Mkoa huo kwa ajili ya kukuza utalii na kuleta maendeleo endelevu

Jumuiya ya Nchi za Ulaya wametoa zaidi ya shilingi Bilioni 3.2 kuendesha mradi huo wa Fahari Yetu ambao utadumu kwa miaka mitatu.

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.