Thursday, February 23, 2017
MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017
- Next You are viewing Most Recent Post
- Previous Denice Simeo Youth Development Expert atoa ushauri kwa vijana wa chuo
google+
There is greatness inside of you
I believe that there is a seed of greatness in all human beings. Therefore the aim of my blog is to bring to my readers awareness of things that are happening around us. I will focus majorly on inspirational news that can motivate my readers to doing more with their lives too. If you are too busy to get acquainted with what is in the newspapers or you have read the papers but have not felt any inspiration or motivation, please log on this page and be inspired to walk in your purpose and dream.
NAMNA UNAVYOWEZA KUPATA MAONO NA KUJUA UNACHOTAKIWA KUFANYA KATIKA KIZAZI CHAKO
a) Kwa njia ya ndoto (unaota ndoto alafu unapata mzigo wa kuona ikitokea) mfano ni Yusufu yeye alikuwa akiota ndoto na akaweka imani yake katika zile ndoto baadae ikawa ni jambo analolitarajia.
b) Kwa njia ya Mawazo (unapata wazo fulani unaanza kulifanyia kazi alafu unashangaa unapata mzigo mkubwa wa kuona ili jambo linatokea.
c) Kwa njia ya elimu ( unapofikia kiwango fulani cha elimu au ufahamu unashangaa kuna kiu inatokea ndani yako juu ya jambo fulani ) hii ilitokea kwa Daniel alipovisoma vitabu akapata ufahamu na huo ufahamu ukampa kiu ya kuona Izrael wanatoka utumwani.
d) Kwa njia ya neno la Mungu ( unasoma neno alafu unasikia shauku ya kuona ulichokisoma kikitokea au ukikifanyia kazi kwa mfumo ambao kinatakiwa kizae jambo fulani.
e) Kupitia watumishi wa Mungu ( unaweza kutolewa unabii au neno la ufahamu na gafra ukaanza kusikia mzigo wa kulifanyia kazi lile lililosemwa na yule mtumishi na baadae linakuja kuwa ni jambo halisi.
f) Kwa kuona watu wengine wakifanya ( unaweza ukaona mtu fulani amefanya jambo fulani gafra ukapata mzigo wa kutamani kufanya na hata ikiwezekana zaidi, kama yeye alienda km 10 wewe unapata mzigo wa kwenda km 15 lakini katika mifumo tofauti, upako tofauti na njia tofauti ( hii tunaiona kwa Musa na Joshua) kwa hivyo basi Mungu anaweza kukuandaa chini ya mtu mwingine bila wewe kujua.
g) Kwa njia ya maombi au Roho mtakatifu ( wapo waliotokewa na Yesu au maraika kwenye maombi na wakaambiwa kazi za kufanya yakawa maono na hatimae yakafanyiwa kazi. Mfano ni Sauli, Manoa Baba yake Samsoni, Mariam na wengine wengi walitokewa na Yesu au Maraika na wakaambiwa yaliyowapasa kuyafanya.
h) Kwa njia ya msukumo wa ndani, unasikia kusoma kozi fulani au unasikia kuanzisha jambo fulani, sasa ukipata nafasi ya kufanya utafiti na kuomba Mungu anakupa njia za kulifanya na ilo jambo na hatimae linakuja linakuwa halisi.
MIFANO KATIKA MAANDIKO namna Baadhi ya watu walivyopata maono
Tumuangalie Mtume Paulo……………
Matendo 9:3-9 anasema “Hata alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafla ikamwangaza kotekote nuru kutoka mbinguni. Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, “Sauli, Sauli, mbona waniudhi?” Akasema u nani wewe, Bwana?”... Naye akasema,“Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe.” Mstari wa sita anaambiwa cha kufanya“Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda” ukisoma mstari wa tisa anasema “Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi”ninachotaka uone ni Namna Sauli alivyopata maono ya kazi iliyokuwa mbele yake na baada ya kuinuka pale alikuwa ni mtu mwingine, akili mpya, mawazo mapya, mipango mipya nk.
Mfano wa pili ni ule wa Neemia alivyopata maono
Nehemia 1:1-4 Ukisoma utaona jinsi ambavyo Nehemia aliuliza habari za wayahudi na Yerusalemu akiwa shushani ngomeni na Hanani akamsimulia yanayoendelea kwa wayahudi ndugu zake jinsi ambavyo walikuwa kwenye dhiki nyingi, na mashutumu; na jinsi ambavyo ukuta wa Yerusalemu ulibomolewa na malango yake kuteketezwa kwa moto. Sasa nataka uone kilichotokea baada ya kusimuliwa hayo mambo, cha kwanza mzigo ukatengenezeka ndani ya Yeremia ukisoma ule mstari wa nne anasema “Hata ikawa niliposikia maneno hayo, nikaketi, nikalia, nikaomboleza siku kadha wa kadha; kisha nikafunga, nikaomba mbele za Mungu wa mbinguni.” Kwa ufupi Nehemia alianza kuomba toba kwa ajili ya wayahudi alafu akapata maono ya kwenda kuujenga tena ukuta wa Yerusalem jambo lililomfanya akaanza kuweka mipango na mikakati, kutafuta vibari ili aende akaijenge tena Yerusalemu na hatimae alifanikiwa kuyatimiza maono yake.
Sasa basi watu wengi sana leo hawajatokewa na malaika kama Manoa wala hawajapata ufunuo kama Sauli isipokuwa wameona uhitaji uliopo na gafra wakapata mzigo na kiu ya kuona wanawajibika kufanya jambo fulani mahala fulani linaweza kuwa la kisiasa au la kibiashara au la kijamii nk. hivyo basi usisubiri mpaka utokewe na Maraika ili kupata Maono maana utachelewa sana angalia nini kinapiga kelele kwenye moyo wako Muombe Mungu alafu atakuelekeza cha kufanya, maana njia ya Mungu ni kamilifu…Zaburi 18:30 anasema“Mungu njia yake ni kamilifu, ahadi ya Bwana imehakikishwa, yeye ndie ngao yao wote wanao mkimbilia.”
Mfano wa tatu ni wa Joshua, tunaona Mungu mwenyewe akimsemesha Joshua na kumpa wajibu mzito ukisoma Yoshua 1:1-3 anasema “Ikawa baada ya kufa kwake Musa, mtumishi wa Bwana, Bwana akamwambia Yoshua, mwana wa nuni, mtumishi wa Musa, akasema, Musa mtumishi wangu amekufa;haya basi,ondoka, vuka mto huu wa Yordani, wewe na watu hawa wote, mkaende hata nchi niwapayo wana wa Israel.”
Ninachotaka uone ni kuwa Joshua alishajifunza mengi kutoka kwa Musa na alishamuelewa Mungu wa Musa hivyo haikuwa ngumu sana juu ya Maono/wajibu huu mpya aliopewa na Mungu kwa habari ya kuanza kuona akiwafikisha wana wa Izrael kule kanani, kwa hivyo basi unaweza ukapata maono kupitia kwa mtangulizi wako, kibiashara, kisiasa, kihuduma nk.
Hii imetokea katika maeneo mengi ya kawaida mfano, Madereva wengi ni wale waliokuwa makondakta baadae wakapata maono ya udereva wakiwa makondakta. Mfano mwingine ni mafundi, wengi ni wale waliokuwa wasaidizi wa mafundi wakuu au walikuwa vibarua wa mafundi wakuu, waimbaji wengi ni wale waliokuwa wacheza shoo au wale waliokuwa wakiwasaidia waimbaji wakuu kuitikia (backup) nk. kwa hivyo unaweza ukapata maono ya jambo lolote lililopo mbele yako kupitia kwa mtangulizi wako.
HAYA NA MENGINE MENGIUTAYAPATA KUPITIA KITABU CHETU CHA NGUVU YA MAONO. Hakikisha unapata nakala yako
Kwa mawasiliano zaidi.
Email:tuntufyemwakyembe@yahoo.com
+255767629562
Arusha. Tanzania
Powered by Blogger.
There is greatness inside of you
I believe that there is a seed of greatness in all human beings. Therefore the aim of my blog is to bring to my readers awareness of things that are happening around us. I will focus majorly on inspirational news that can motivate my readers to doing more with their lives too. If you are too busy to get acquainted with what is in the newspapers or you have read the papers but have not felt any inspiration or motivation, please log on this page and be inspired to walk in your purpose and dream.