SABABU ZA UMUHIMU WA KUOMBA JUU YA KUSUDI LA MUNGU KWENYE MAISHA YAKO | Apostle Darmacy Blog MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 | Apostle Darmacy Blog

APOSTLE DAMAS

Breaking News

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, February 23, 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 

 

Goo

 

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 
About Muses Radio Player...
Version 2.1 (html5)

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.
-->

Tangaza nasi

Breaking News
Loading...

Soma App

Soma App
DOWNLOAD Somaapp NOW!

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Tuesday, October 18, 2016

SABABU ZA UMUHIMU WA KUOMBA JUU YA KUSUDI LA MUNGU KWENYE MAISHA YAKO



Ø  Lengo ni kuwa endapo ibilisi atakuwa amepanda  kitu cha kwake au mataifa wamekunasa na vitu ambavyo si kusudi la Mungu kwako na wewe kufikiri ndio Mungu anataka, vitu ivyo vibatilishwe na nguvu ya Mungu. Zab 33:10 anasema “BWANA huyabatilisha mashauri ya mataifa huyatangua makusedi ya watu” mstari wa 11 anasema “Shauri la BWANA lasimama milele, makusudi ya moyo wake vizazi na vizazi” hivyo maombi yatabatilisha makusudi ya watu.
Ø  Unapoomba endapo ulikuwa umenaswa katika hali ya udanyanyifu na moyo wako kudhania kuwa hivyo ndivyo ulivyopaswa kwenda nguvu ya maombi hutangua mipango ya udanyanyifu na kutembea kwenye kusudi hasa uliloitiwa, Ayubu 5:12 anasema “Yeye huyatangua mashauri ya wadangenyifu, mikono yao isipate kuyatimiza makusudi yao”
Ø  Unapojikabidhi kwa Mungu na mipango yako anakusaidia kutembea kwenye kusudi lake Mith 16:3 anasema “Mkabidhi Bwana kazi zako na mawazo yako yatadhibitika” ukisoma Biblia ya kingereza tafsiri ya Good News anasema “Ask the LORD to bless your plans and you will be successful in carring them out” akiwa na maana muombe Mungu abariki mikono yako ili ifanikiwe, hivyo basi ni vema ukaelewa kuwa bila Mungu kukuwezesha huwa haiwezekani kufanikiwa kutembea kwenye kusudi lake ndio sababu ukisoma Mith 16:9 utakuta anasema “Moyo wa mtu huifikiri njia yake; bali Bwana huziongoza hatua zake” Ikiwa na maana unaweza ukafikiri ukawana maono na usiongozwe na Bwana lakini pia unaweza ukafikiri ukaomba ukawana maono na ukaongozwa na Bwana.
Ø  Maombi hufungua macho husaidia kupata ufahamu na unapokaa kwenye maono ni rahisi kujua ni nini hasa wito wako, kusudi la Mungu kukuitwa hapo na hata amani tumaini kutawaka moyoni mwako, ukisoma Efeso 1:18 anasema “Mcho ya mioyo yenu yatiwe nuru mjue tumaini la mwito wake jinsi lilivyo; na utajiri wa utukufu wa urithi wake katika watakatifu jinsi ulivyo………”
Ø  Maombi humpa nafasi roho mtakatifu kukusaidia wewe kuwa na uhakika wa mahali ulipo na kitu unachokifanya, ndio sababu kama uka njia panda huelewi cha kufanya huna amani usihangaike na hiyo hali isipokuwa ingia kwenye maombi Filipi 4:6 anasema “Msijisumbue kwa neno lolote; bali katika kila neon kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu zijulikane na Mungu” Matokeo ya maombi itakuwa ni Amani na Mungu kukusaidia kukaa mahali sahihi na kwenye lengo sahihi, ukiendelea anasema
“Na amani ya Mungu, ipitayo akili zote,itawaifadhi mioyo yenu na nia zenu katika Kristo Yesu”  
Ø  Maombi hutusaidia kushinda vikwazo na majaribu mbali mbali maana inawezekana kabisa mahali ulipo ni sahihi isipokuwa unahitaji kuomba ili kuwa na uhakika pia kushinda vikwazo mbali mbali Math 26:41 anasema “ Kesheni, muombe, msije mkaingia majaribuni……” katika kiingereza tafsiri ya Good News ni nzuri zaidi anasema “Keep watch and pray that you will not fall into temptation” hii ukitafsiri katika Kiswahili ana maana kuweni waangalifu msije mkaangukia majaribuni ikiwasisitiza kuomba wasije wakashindwa majaribu yatakayokuja kwa hiyo maombi yanakusaidia kuwa na nguvu ya kutosha kukabiliana na vikwazo hasa unapokuwa unalitimiza kusudi.
Ø  Maombi yatakusaidia kujua fikra na mipango ya adui katika kukuzuia usilifikie lile ambalo Mungu amelikusudia, maana unaweza ukawa mahali sahihi lakini usiweze kulifikia lile lililokusudiwa  ukisoma 2Korintho 2:11 anasema “Shetani asije akapata kukushinda; kwa maana hatukosi kuzijua fikra zake” Hivyo maombi ni taa na macho ya kukusaidia kuiona na kuitambua mipango ya adui ili asije akatushinda.
Ø  Maombi hutisaidia kushinda mitego mbali mbali ya mwovu, mara nyingi utakapotembea kwenye kusudi, ibilisi atakupiga maana anajua unaujenga ufalme wa Mungu na hivyo kutakuwa na mitego mbali mbali ya adui kukutoa katika kulitimiza kusudi la Mungu ukisoma Zab 91:3 anasema “Maana yeye atakuokoa na mitego ya mwindaji………” hivyo basi kuna umuhimu wa kujipanga kwenye maombi has unapojua lipo kusudi unalitimiza.
Ø  Maombi yatakusaidia kufanya maamuzi sahihi ili uweze kulitimiza kusudi la Mungu, unapohitaji kujua nini ufanye, wapi ni sahihi kwako, yupi atakuwa ni mume sahihi kwako, mke sahihi haya na mengine mengi ni mambo yanayohitaji kufanya maamuzi sahihi nje ya hapo hutafanikiwa katika kulitimiza kusudi la Mungu alilokuitia hebu tujifunze kwa Bwana Yesu, unaposoma Luka 6:12 anasema “Ikawa siku zile aliondoka akaenda mlimani ili kuomba, (Huyu ni Bwana Yesu) akasesha usiku kucha katika kumwomba Mungu hata ilipokuwa mchana aliwaita wanafunzi wake; akachagua kumi na wawili miongoni mwao, ambao aliwaita mitume” kumbe ili kufanya maamuzi sahihi unahitaji muda wa kutosha kumwomba Mungu Bwana Yesu alikesha usiku kucha akimwomba Mungu ili asikosee katika kuchagua, wewe je! utahitaji muda gani?
Ø  Maombi yatakusaidia kuendelea kukua na kuishi katika hali ya hekima na maarifa na ufahamu wa kimungu ili kuendelea  kuujenga ufalme wa Mungu  ukisoma Kolosai 1:9 anasema “Kwa sababu hiyo sisi nasi, tangu siku ile tuliposikia, hatuachi kufanya maombi na dua kwa ajili yenu, ili mjazwe maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa rohoni” kumbe ni maombi yanayoweza kumjaza mtu maarifa, hekima na ufahamu wa rohoni.
Maombi yatakusaidia kuendelea kuishi kwa Imani pasipo kusitasita, Ebrania 10:38 anasema “Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa Imani nae akisitasita roho yangu haina furaha nae”
Ø  maombi huuwa matendo ya mwili (tamaa mbaya, uadui, fitina na mengineyo mengi) ukisoma Rumi 8:10 anasema “Na Kristo akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa sababu ya dhambi; bali roho yenu I hai kwa sababu ya haki” na ukisoma katika Galatia 5:24 anasema “Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulubisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya na tamaa zake” Unausulubishaje ni kwa maombi na kuutafuta uso wa Mungu.
Ø  Maombi yatakusaidia kupata ufunuo Ukisoma Ufunuo 2:9 anasema “ Lakini kama ilivyoandikwa mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu, mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa roho” Sisi ambao tumelibeba kusudi lake.
Ø  Maombi yatakusaidia katika udhaifu alio nao, mapungufu yako, ukisoma Rumi 8:26 anasema “ Kadhalika roho nae hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi ipasavyo; lakini roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua tusikoweza kutamkwa” Neno udhaifu kwenye tafsiri ya kingereza limeandikwa Weakness yaani Mapungufu, hivyo usipokuwa muombaji hakuna namna unaweza kupona na mapungufu ulionayo, unapoomba kwa muda wa kutosha unatoa nafasi ya roho  mtakatifu kukusaidia, maana ibilisi anaweza kutumia mapungufu ulionayo kukuvuruga.
Ø  Maombi yatakusaidia kuitunza nafasi yako 1Timoth 5:6 “Basi yeye asiyeizuia nafsi yake amekufa ingawa yu hai” ukisoma Tito 1:8 anasema “Bali awe mkaribishaji, (huyu mtumishi aliyebeba kusudi la Mungu) mpenda wema mwenye kiasi, mwenye haki, mtakatifu, mwenye kuidhibiti nafsi yake” kumbuka utatakiwa kudhibiti nafsi yako maana kuna wakati nafsi itakutaka uishi kwa kufuata tama za mwili na zile za duniani, sasa ni maombi peke yake yatakayoweza kukusaidia kuidhibiti na si vinginevyo.
Ø  Usiache kuombea kutimilika kwa kusudi la mungu kwenye maisha yako yaani kuufikia mwisho mwema, Mtume Paulo alifanikiwa kulijua  kusudi la Mungu kwenye maisha yake na hatimaye kuufikia mwisho mwema. 2 Timoth 4:7 anasema “Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda…” ni maombi yangu kuwa uje useme maneno kama haya utakapokuwa ukimaliza wito wako.
Daudi pia alilitimiza kusudi la Mungu vizuri maishani mwake na kuufikia mwisho mwema unaposoma Matendo 13:36 anasema “Kwa maana Daudi, akiisha kulitumikia shauri la Mungu katika kizazi chake, alilala (Ahaa! kumbe ukulitimiza kusudi la Mungu haufi isipokuwa unalala maana kuna siku utaamshwa) akawekwa pamoja na Baba zake….”
MAMBO YA KUFAHAMU KUHUSIANA NA KUSUDI LA MUNGU
Ø  Ukiishi nje ya mpango wa Mungu kuna Baraka hutaweza kuziona maishani mwako.
Ø  Ukiishi nje ya mpango wa Mungu kuna hatari ya kuishia kwenda jehanamu.
Ø  Ukiishi kwenye mpango wa Mungu ni mtaji wako wa kuurithi uzima wa milele.
Ø  Mungu alituumba ili tumzalie matunda na si vinginevyo.
Ø  Hakuna aliyeumbwa bila kitu/kipawa unatakiwa tu kuomba ili ujue namna ya kufanya.
Ø  Unapomtumikia Mungu anakuheshimu.
Ø  Wanaoishi sawa na mpango wa Mungu wanapata upendeleo kwa Bwana.
Ø  Kuishi sawa sawa na mpango wa Mungu unakuwa ni mtenda kazi pamoja na Kristo.
Ø  Kuishi nje ya kusudi unaweza kusababisha ghadhabu ya Mungu kwenye maisha yako maana alikuleta kwa kazi maalum.
MASWALI AMBAYO UNATAKIWA KUJIULIZA
           i.            Niliubwa kwa ajili ya nini? Na je nalitimiza lengo la Mungu kuniumba?
         ii.            Ni nini lengo kuu la Mungu kuniweka hai leo?
       iii.            Je ninaishi kwa faida ya Mungu? Au ya Ibilisi?
       iv.            Mungu anataka nini kwenye maisha yangu?
         v.            Je maisha yangu yana mchango wowote katika jamii katika kuujenga Ufalme wa Mungu?
       vi.            Je ninafanyika Baraka mbele za Mungu na watu wanaonizunguka?
     vii.            Ni kitu gani kinaniongoza kwenye maisha yangu?
   viii.            Je! maisha yangu yanawaidia wengine kupata tumaini katika wito walioitiwa?
       ix.            Je! ni kitu gani kinachonizuia kuishi sawa na mpango wa Mungu?
         x.            Je! ninamruhusu Mungu kunitumia au namzuia kwa jinsi nilivyo?
       xi.            Je! nina muda wa kutosha kutafakari mwisho wangu?
     xii.            Je! nina sifa za kutumiwa na Kristo! kama chombo chenye heshima?
   xiii.            Je! ni vitu gani vinaweza kuchochea zaidi wito ulioko ndani yangu?
    xiv.            Na Je! ni vitu gani vinaweza kuharibu wito nilionao?
      xv.            Je! nimejitoa kwa Mungu kwa jinsi anavyotaka?
    xvi.            Naweza kuwa nasonga mbele! nimesimama au narudi nyuma katika kuutimiza wito nilioitiwa?
  xvii.            Na je! hivi nilivyo ndivyo Mungu anavyotaka niwe?
Unapopata nafasi ya kujihoji namna hii itakusaidia kujipanga na Mungu kwa mfamo ambao utakusaidia kusonga mbele ili kulitumikia  kusudi lake alilotuitia.
Mwl. Tuntufye A. Mwakyembe
Tuntufyemwakyembe@yahoo.com
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.