Clinton Na Trump Wajinadi Dakika Za Mwisho | Apostle Darmacy Blog MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 | Apostle Darmacy Blog

APOSTLE DAMAS

Breaking News

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, February 23, 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 

 

Goo

 

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 
About Muses Radio Player...
Version 2.1 (html5)

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.
-->

Tangaza nasi

Breaking News
Loading...

Soma App

Soma App
DOWNLOAD Somaapp NOW!

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Monday, November 7, 2016

Clinton Na Trump Wajinadi Dakika Za Mwisho


Hillary Clinton na Donald Trump wamefanya mikutano ya dakika za mwisho mwisho kuwahimiza raia wa Marekani wawapigie kura zikiwa zimesalia saa chache kabla ya uchaguzi kufanyika.
Wote wawili wamefanya mikutano ya kampeni katika majimbo ya kushindaniwa ya Carolina Kaskazini, Pennsylvania na Michigan.
Bi Clinton amewahimiza wapiga kura kuunga mkono kuwepo kwa “Marekani yenye matumaini, inayojumuisha wote na yenye ukarimu”.
Bw Trump naye amewaambia wafuasi wake kwamba wana “fursa nzuri ya kuvunja mfumo mbovu na usio na maadili”.
Kura za maoni zinaonesha Bi Clinton wa chama cha Democratic akiwa asilimia nne mbele ya mpinzani wake Bw Trump wa chama cha Republican.
Wapiga kura wengi kuliko awali, zaidi ya 46 milioni, tayari wamepiga kura za mapema.
Kuna ishara za wapiga kura wa asili ya Kihispania (Latino/Mexico) kujitoleza kwa wingi, jambo ambalo wengi wanaamini litamfaa Bi Clinton.
Uchaguzi mkuu unafanyika baada ya kampeni kali ambapo wapiga kura walirushiana matusi na kila mmoja alikabiliwa na kashfa.
Kwenye hafla Philadelphia, Pennsylvania, Bi Clinton ameungana na nyota Bruce Springsteen na Jon Bon Jovi jukwaani pamoja na mumewe Bill, Rais Obama na mkewe Michelle.
Bw Obama amewataka wapiga kura kukataa kutawaliwa na woga na badala yake waamue kukumbatia matumaini.
_92317026_mediaitem92317025







Mkutano wa mwisho wa kampeni wa Bi Clinton ulikuwa Raleigh, Carolina Kaskazini, ambao angemshirikisha Lady Gaga.
Awali, alisema kwenye mahojiano redioni kwamba akishinda atampigia simu Bw Trump na kwamba anatumai mgombea huyo wa chama cha Republican anaweza “kutekeleza mchango muhimu” katika kuunganisha tena taifa hilo.

Bw Trump, kwenye mkutano wake wa kampeni mjini Scranton katika jimbo hilo alisisitiza kwamba kampeni yake imekuwa ikiimarika.
Mkutano wake wa mwisho ulikuwa Grand Rapids, Michigan.
Awali, aliwaambia wafuasi wake jimbo la Florida kwamba yeye “si mwanasiasa” na kwamba anawajali wao pekee.
Mfanyabiashara huyo alimweleza Bi Clinton kama “mtu mwovu zaidi aliyewahi kuomba kuchagulikuwa kuwa rais”, akirejelea uchunguzi wa FBI kuhusu hatua ya Bi Clinton ya kutumia sava ya kibinafsi ya barua pepe kutuma barua pepe rasmi alipokuwa waziri wa mambo ya nje kati ya 2009 na 2013.
Jumapili, Bi Clinton alipata nafuu baada ya FBI kusema barua pepe mpya zilizokuwa zimegunduliwa kwenye uchunguzi mwingine hazikutoa ushahidi wowote wa kumpata na hatia.
_92317030_mediaitem92317029


Hayo yakijiri, meneja wa kampeni wa Bw Trump, Kellyanne Conway amepuuzilia mbali wasiwasi miongoni mwa jamii ya kimataifa kuhusu uwezekano wa mgombea huyo wa Republican kushinda.
Akiongea na BBC Jumatatu, alisema ukosoaji ambao umekuwa ukitoka nje ya nchi “hauashirii sifa halisi za Donald Trump na sababu zinazomfanya awanie urais na sifa atakazokuwa nazo jukwaa la kimataifa akishinda”.
Rais wa Ufaransa Francois Hollande alikuwa amesema bilionea huyo humfanya “ahisi kutapika”.
Bw Trump amekabiliwa na shutuma kali hasa kutokana na madai ya kuwadhalilisha kingono wanawake, madai ambayo Bw Trump ameyakanusha.
Aidha, kuna kadha zilizotolewa zikimuonesha akitoa matamshi ya kuwadhalilisha wanawake. Bw Trump alisema mazungumzo hayo yalikuwa ya mzaha na ya faraghani.
Bw Trump pia ametuhumiwa kwa kueneza chuki dhidi ya wageni baada ya kuapa kuwapiga marufuku Waislamu wasiingie Marekani kwa muda kama njia ya kukabiliana na ugaidi.
Aliwaeleza raia wa Maexico kuwa “wabakaji” na kadhalika, alisema angejenga ukuta kwenye mpaka wa Marekani kuwazuia Wamarekani wasiingie nchini humo.
Credit to

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.