Uelewa wa saratani ya tezi dume- (Prostate gland) | Apostle Darmacy Blog MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 | Apostle Darmacy Blog

APOSTLE DAMAS

Breaking News

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, February 23, 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 

 

Goo

 

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 
About Muses Radio Player...
Version 2.1 (html5)

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.
-->

Tangaza nasi

Breaking News
Loading...

Soma App

Soma App
DOWNLOAD Somaapp NOW!

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Monday, November 7, 2016

Uelewa wa saratani ya tezi dume- (Prostate gland)


Maana, dalili, vipimo na matibabu ya tezi dume.



Tezi Dume (Prostate gland)
Tezi dume ni sehemu mojawapo ya mfumo wa uzazi wa kiume. Inaundwa na sehemu mbili, lobes, ambazo zimeunganishwa na kufunikwa kwa nje kwa utando wa tishu. Tezi hii ipo mbele kidogo ya puru (rectum) na na chini kidogo ya kibofu cha mkojo. Tezi dume inauzunguka mrija unaounganisha kibofu cha mkojo na uume (urethra).

Mojawapo ya kazi za tezi dume ni kutoa majimaji yanayochanganyika na mbegu za kiume (sperms) wakati wa kilele cha tendo la ngono. Mchanganyiko huu wa mbegu pamoja na majimaji hayo hufanya shahawa (semen). Aidha majimaji hayo husaidia kuzipa mbegu za kiume nguvu ya kusafiri kwenye uke mpaka kufikia kwenye mirija ya fallopian tayari kwa utungisho na yai la kike. Vilevile husaidia kupunguza hali ya kitindikali iliyopo katika uke, ambayo kama isiporekebishwa, huweza kuua mbegu nyingi za kiume na kufanya utungisho kuwa wa tabu.

Kuvimba Tezi Dume (BPH)
Kwa kadiri mwanaume anavyozeeka, ni jambo la kawaida pia kwa tezi dume kuongezeka ukubwa na kuvimba. Hali hii kitabibu huitwa Benign Prostate Hyperplasia au wengine hupenda kutumia maneno Benign Prostate Hypertrophy kwa kifupi BPH. Kwenye makala hii tutautumia sana ufupisho huu wa BPH ili kurahisisha mambo.

Ukuaji wa tezi dume hupitia hatua kuu mbili. Hatua ya kwanza hutokea kipindi cha balehe wakati tezi dume linapoongezeka ukubwa na kuwa mara mbili ya lilivyokuwa hapo awali. Baada ya hapo ukuaji husimama kwa muda mpaka kijana anapofikisha miaka 25 hadi 30 ndipo hatua ya pili ya ukuaji huanza tena. Ukuaji huendelea kwa viwango na kasi tofauti kati ya mtu na mtu na hatimaye kusababisha
BPH katika umri wa utu uzima.

Wakati tezi dume linapokua na kutanuka, utando wa tishu unaozulizunguka hutanuka pia. Hata hivyo ingawa tezi dume huendelea kukua, hufikia wakati utando wake huacha kutanuka na kufanya tezi dume kubana mrija wa kutolea mkojo kutoka kwenye kibofu. Hali hii husababisha kibofu cha mkojo kuwa na ngozi ngumu. Hali hii hufanya kibofu cha mkojo kuhisi kutaka kutoa mkojo nje hata kama kiasi cha mkojo ndani yake ni kidogo sana. Hufikia wakati, kibofu huwa dhaifu na kupoteza uwezo wake wa kuhisi kutoa mkojo na hivyo kufanya mtu anapokojoa kushindwa kutoa mkojo wote na badala yake hubakiza kiasi fulani cha mkojo kwenye kibofu.

BPH husababishwa na nini?
Chanzo halisi cha BPH au vihatarishi vyake (risk factors) havijulikani kwa uhakika. Kwa muda mrefu imekuwa ikichukuliwa kuwa BPH hutokea kwa wanaume watu wazima na wazee tu. Aidha imewahi kuonekana huko nyuma kuwa PBH haitokei kwa wanaume ambao wamewahi kufanyiwa operesheni ya kuondoa korodani au wale ambao walizaliwa bila korodani. Hali imepelekea baadhi ya watafiti kuamini kuwa BPH ina uhusiano mkubwa na umri wa mtu pamoja na uwepo wa korodani.

https://www.youtube.com/watch?v=a02_mY2ucDg

Makala ha hapa chini  imeandikwa na Asha Bani


NILIWAHI kuandika makala kuhusiana na saratani ya tezi dume baada ya kufanya mahojiano na mwathirika wa ugonjwa huo, Dk. Emmauel Kandusi.
Kupitia makala ile ambayo alieleza namna ugonjwa huo ulivyo hatari kwa taifa, wengi walijitokeza kutaka kujua dalili na hali hatarishi za ugonjwa huo.
Ingawa nilifanikiwa kuwaunganisha na Dk. Kandusi mwenyewe kwa maelezo zaidi, kwa wengine nilishindwa kufanya hivyo.
Kwa mazingira hayo, natumia nafasi hii kueleza mambo kadhaa yahusuyo ugonjwa huo, nikiamini kama si kuyamaliza, basi nitakuwa nimepunguza maswali ya wengi.
Nitakachofanya ni kuweka namba ya mawasiliano ya Dk. Kandusi ili waweze kuwasiliana naye moja kwa moja kwa ushauri zaidi.
Dk. Kandusi anaanza kuelezea maana ya saratani kwamba ni jina la ugonjwa ambalo hutokea wakati chembechembe za uhai katika sehemu fulani ya mwili zinapoanza kukua bila kufuata utaratibu na mfumo wa mwili.
Chembechembe hizi huasi na kutengeneza vivimbe vidogo vidogo.
Lakini kwa kuwa yeye ni muathirika wa saratani ya tezi dume, anauelezea kwa undani ugonjwa huo unaosumbua watu wa jinsia ya kiume.
Anasema saratani ya tezi dume ni ugonjwa unaopatikana katika mwili wa kiumbe mamalia dume tu, ambapo chembechembe za uhai katika tezi dume zinakua bila kufuata utaratibu na mfumo wa mwili.
Hizo huasi na kutengeneza vivimbe vidogo vidogo na mtu kuwa amethirika.
Hali hatarishi
Dk. Kandusi anasema kuna hali hatarishi nyingi ambazo zinachangia mwanamume kupata saratani ya tezi dume, ikiwa ni pamoja na umri ukifikia miaka 50 na kuendelea.
Nasaba
Kama katika ukoo kuna historia ya ugonjwa wa saratani ya tezi dume, suala la nasaba linachangia kumweka mwanamume kuwa hatarini kuathirika na saratani hiyo kwa misingi ya kinasaba ‘genetic.’
Lishe
Ananasema wanaume wanaopenda kula nyama nyekundu ‘red meat’ yenye mafuta mengi na aina ya maziwa yenye mafuta mengi wako katika hali hatarishi ya kuathirika.
Mazoezi
Kama mwanamume hafanyi mazoezi na ana unene hatarishi, sambamba na ukosefu wa virutubisho D, ana uwezekano mkubwa wa kuugua ugonjwa huo.
Dalili za saratani ya tezi dume
Dk. Kandusi anasema kuwa kuna dalili nyingi za saratani ya tezi dume, ikiwa ni pamoja na udhaifu katika kujisaidia haja ndogo na pindi inapopatikana, inakuwa ni ya kukatiza katiza.
Kushindwa kukojoa na kushindwa kuanza kupata haja ndogo huku unapohisi haja ndogo unapata shida pia kujizuia isitoke yenyewe.
“Hisia ya kutaka kupata haja ndogo na hata wakati mwingine kwa usiku unaweza ukakojoa kitandani, pia unaweza ukapata maumivu na kuhisi mwasho wakati wa haja ndogo,” anasema Dk. Kandusi.
Anasema hii ni kutokana na uume kusimama kwa shida na hata maumivu makali pindi anapotoa manii wakati wa kujamiiana.
Anasema dalili nyingine ni kuwapo kwa damu damu wakati wa kukojoa na katika manii, huku kukiwa na maumivu ya viungo, ikiwa ni pamoja na kiuno, miguu na mgongo.
Pia anaeleza kuwa mgonjwa anaweza kukosa hamu ya kula na kupungua uzito.
Dk. Kandusi anasema pamoja na kuelezea dalili za ugonjwa huo, lakini mwanamume anapoanza kuziona na kuzihisi kati ya dalili hizo, ni lazima ajue kuwa chembe chembe za uhai hasi katika tezi dume lake zina umri wa takriban miaka saba na kuendelea.
Uchunguzi
Anatoa wito kwa wanaume wenye umri wa takriban miaka 50 na kuendelea kuweka kipaumbele tabia ya kufanyiwa uchunguzi wa tezi dume angalau mara moja kwa mwaka.
Vipimo
Kuna vipimo vya uchunguzi wa tezi dume kama vipimo ashiria, kitaalamu ‘Prostate Specific Antigen (PSA) na Digital Rectal Examination (DRE), kwa mujibu wa Dk. Kandusi.
Tiba
Anasema kuna tiba za aina nyingi, ikiwa ni pamoja na ya uangalizi (active surveillance), upasuaji (surgery) homoni (hormonetherapy), mionzi (radiotherapy), dripu kemikali (chemotherapy) na kama ikigundulika una saratani dume unatakiwa kushauriana na daktari wako ni tiba ya aina ipi inatakiwa kufanyika kati ya hizo.
Pia Dk. Kandusi anatoa wito kwa wanaume wote wenye umri wa miaka 50 na kuendelea wanapopatwa na ugonjwa wa aina yoyote ni vema wakapimwa na saratani ya tezi dume.
Pia anasema kila mtu anatakiwa kutambua kuwa saratani ikigundulika mapema ni rahisi kutibika.
Hata hivyo, hivi karibuni kikundi cha 50 Campaign walifanya uzinduzi wa harambee ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kununua basi litakalotumika katika kampeni ya kuhamasisha watu dhidi ya ugonjwa huo, harambee iliyoendeshwa na raia wa Boston, Shedmin Luvanda, ambaye alikabidhi hundi ya dola za Marekani 5,000 ambazo zilichangwa na yeye na marafiki zake wa Boston.
Lengo ni kukusanya kati ya sh milioni 45 na sh milioni 126 kwa ajili ya kununua gari jipya au lililotumika.
Kutokana na ugonjwa huo kuwa hatari hapa Tanzania, ifikapo mwaka 2020 unatarajiwa kuua watu milioni 20, hivyo Dk. Kandusi anaomba taasisi na watu binafsi kuchangia fedha kwa ajili ya kununulia gari na masuala mengine ya vipimo na matibabu.
Anasema ili kufanikisha mpango huo, mtu anaweza kuchangia kwa M- Pesa namba 0754 402033 au kupitia akaunti namba 01J1027311100 katika tawi lolote la CRDB, ikiwa na jina la akaunti ‘Center for Human Rights Promotion –CHRP’

0788 150 928
Makala imeandikwa na Asha Bani

Source: Tanzania Daima

 




Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.