Maombi ya kushindana na kujinasua toka mikono ya adui-Mwl.Tuntufye A. Mwakyembe | Apostle Darmacy Blog MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 | Apostle Darmacy Blog

APOSTLE DAMAS

Breaking News

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, February 23, 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 

 

Goo

 

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 
About Muses Radio Player...
Version 2.1 (html5)

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.
-->

Tangaza nasi

Breaking News
Loading...

Soma App

Soma App
DOWNLOAD Somaapp NOW!

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, February 23, 2017

Maombi ya kushindana na kujinasua toka mikono ya adui-Mwl.Tuntufye A. Mwakyembe

HATUA 12 KATIKA MAOMBI YA KUJIFUNGUA KUTOKA KATIKA VIFUNGO MBALIMBALI NA NAMNA YA KUOMBA.
Image may contain: 9 people, people standing and crowd
Mwl.Tuntufye A. Mwakyembe

 
     1.     Unapotaka kuomba maombi haya hakikisha unaamini kuwa Mungu yupo na kuwa anazo nguvu za kukufungua hata ukiomba wewe mwenyewe….Isaya 61:1 aya ni maneno ya Bwana Yesu “Roho ya Bwana Mungu i juu yangu, kwa sababu Bwana amenitia mafuta, niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma ili kuwaganga waliovunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao.”
 
2.     Amini kuwa Mungu huwapa thawabu wale wamtafutao kwani Maandiko yanasema katika … Ebrania 11:6 b kuwa “Kwa maana mtu amwendeae Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.” Kama ukiamua kumtafuta amehaidi kukusaidia

3.     Omba huku ukiamini Mungu anakwenda kukufungua, kukuweka huru, kukujibu mahitaji yako…  Ebrania 10:38  “Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; naye akisitasita, roho yangu haina furaha naye”.
kumbuka msingi mkubwa wa maombi haya ni kuamini, ukisita sita Mungu hana furaha nawe.

4.     Kwenye Moyo wako tengeneza shauku ya kuutua mzigo wako kwa Yesu, iwe ni hamu yako iwe ni haja yako, pia  iwe ni matamanio yako …Math 11:28 anasema “Njoni kwangu ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha…” Hakuna mwanadamu anayeweza kuutua mzigo wako isipokuwa Bwana Yesu

5.     Tubu kwani inawezekana umehusika kwa namna moja ama nyingine kumpa ibilisi nafasi ya kukunyanyasa, na kama hujahusika tubu kwa ajili ya waliohusika ikiwa unawajua, inaweza kuwa wazazi au ndugu wa karibu Mungu atasamehe …Isaya 43: 25 “Mimi, naam, mimi,Ndimi niyafutae makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako” Ukitubu kwa kweli Mungu amesema hata zikumbuka dhambi zako na hivyo utakuwa na ujasiri wa kuendelea kusogelea kusogelea madhabahu yake kwa maombi

6.     Wasamehe wote waliosababisha mateso na uchungu kwenye maisha yako…Math 6:14 “Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao Mungu wa mbinguni atawasamehe ninyi makosa yenu… Marko 11:26 “Lakini kama ninyi hamsamehe, wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.”  Kumbuka kisasi ni juu ya Bwana samehe alafu mwambie Bwana Yesu akufungue.

7.     Omba kwa kukiri ukitamka kwa kinywa chako… Warumi 10:10 “Kwa maana kwa Moyo mtu huamini hata kupata haki,  na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu” pia ukisoma  Mithali 18:21 anasema “Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi; nao waupendao watakula matunda yake” tumia kinywa chako kukiri uzima, omba kwa kutamka, tafuta mazingira ambayo hauta msumbua mtu mwingine, tamka kwa kinywa chako Ushindi, mafanikio , uzima huku ukikemea yale usiyoyataka na Mungu atafanya.

8.     Omba kwa kutumia Damu ya Yesu … Ufunuo 12:11 “Nao wakamshinda kwa Damu ya mwana kondoo...” Damu ya Yesu inatupa ushindi pia ukisoma …Isaya 53:5 anasema  “Bali alijeruhuwa kwa makosa yetu alichubuliwa kwa maovu yetu adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.” Ukiendelea katika  1petro 1:18a-1 Ninyi mfahamu kuwa mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo bali kwa Damu ya thamani kama ya mwanakondoo asiye na hila asiye na waa yaani kristo. Kwa hivyo amini kabisa kuwa ipo Damu ya Yesu itakayo kusaidia kushinda maana anasema wakamshinda kwa Damu ya mwana kondoo.

9.     Omba kwa kutumia Jina la Yesu… Yoh 14:14 “Mkiomba  neno lolote kwa jina langu, nitalifanya.”  Pia ukisoma Marko 16:17 “Na Ishara hizi Zitafuatana na hao waaminio: kwa jina langu watatoa pepo  watasema kwa lugha mpya…” Hakikisha maombi yako yanajengeka katika misingi ya jina la Yesu…tumia jina la Yesu kukemea, kuomba na katika kila hali ya kuitaji msaada toka kwa Mungu.

10.                        Tumia moto wa Roho Mtakatifu… wakati mwingine kwenye maandiko umejulikana kama moto ulao… Eliya aliwahi kuamuru Moto toka Mbinguni ukashuka na kuteketeza Askari waliokuwa wametumwa na mfalme dhidi yake…2Wafalme1:10  “Eliya akajibu akamwambia Yule akida wa hamsini ikiwa mimi ni mtu wa Mungu na ushuke Moto kutoka Mbinguni ukuteketeze wewe na hamsini wako Moto ukashuka ukawateketeza yeye na hamsini wake”.  lakini pia aliamuru Moto ushuke nao ukashuka na kuteketeza sadaka… Falme 18:37 Unisikie ee Bwana unisikie ili watu hawa wajue ya kuwa wewe Bwana  ndiwe Mungu na kuwa wewe unawageuza moyo wakurudie ndipo Moto wa Bwana ukashuka ukateketeza sadaka ya kuteketezwa na kuni na mawe na mavumbi ukayaramba yale  maji  yaliyokuwemo kwenye mfereji…Elewa wazi kabisa kuwa unao uwezo wa kushusha moto hata kama hautauona kwa macho ya kibinadamu lakini lakini uwe na uhakika utateketeza na kuharibu vitu vya adui katika ulimwengu wa roho.

11.                        Tumia Neno la Mungu maana li hai tena lina nguvu Ebrania 4:12 anasema “Maana neno la Mungu li hai, tena lina nguvu, tena lina ukali kuliko upanga uwao wote ukatao kuwili; tena lachoma hata kuzigawanya nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake;  tena lijepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo, wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu. Hivyo basi uwapo katika maombi haya tumia neno la Mungu kudai ukombozi wako ndio sababu pia ukisoma  Yeremia 1:12 anasema “Ndipo Bwana akaniambia, umeona vema, kwa maana ninaliangalia neno langu, ili nilitimize.” Hakikisha unasimamia ahadi za Mungu kila unapoomba na mkumbushe Mungu kupitia ahadi zake.

12.                        Shugulikia chanzo cha tatizo kwa maombi chanzo cha tatizo chaweza kuwa Roho za upatilizo / kurithi …wapo waliorithi uchawi, magonjwa, mikosi na mabalaa, kutokufanikiwa, ufukara, utasa na mengineyo mengi. Kutoka 20:5b anasema “Nawapatiliza wana maovu ya Baba zao…” Hivyo basi kuna mabaya unayapitia tu kwa sababu ya wazazi wako au watu wa ukoo wako waliopita… pia ukisoma Maombolezo 5:7 anasema “Baba zetu walitenda dhambi hata hawako, na sisi tumeyachukua maovu yao” kataa na ujitenge na kila uovu wa nyuma kwa jina la Yesu kwa Damu ya Yesu na kwa Moto wa Roho Mtakatifu ndio sababu ukisoma   Zab 11:3 anasema “Kama misingi ikiharibika, mwenye haki atafanya nini?” Unaweza kuwa una haki lakini ulitolewa kwa mizimu au kwa nguvu za giza lazima ujue na ujinasue kwa maombi kataaa kabisa hali yoyote ya kuhusishwa na mambo ya kurithi..toka katika familia na ukoo kwa namna ya magonjwa, mikosi na mabalaa.
 Elewa kuwa unashugulika na Ulimwengu usio onekana ( ulimwengu wa Roho)   hivyo ni lazima kujipanga kwa maombi na neno la Mungu.
Efeso 6:12 anasema “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho”
Kwa hivyo basi pata muda wa kuomba kila wakati maana unapoomba unampa Mungu nafasi ya kukusaidia na kukutetea katika mambo mengi ambayo unayahitaji kila wakati.

Kwa mawasiliano zaidi.
Mwl.Tuntufye A. Mwakyembe
+255767629562
+255715629562
Arusha. Tanzania
Pia waweza kutufuatilia kupitia
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.