Day 2: Semina ya Neno la Mungu Dodoma- " Fahamu Ya yafuatayo kuhusu Ndoto unazoota ili ufanikiwe kimaisha" Mwl. Mwakasege | Apostle Darmacy Blog MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 | Apostle Darmacy Blog

APOSTLE DAMAS

Breaking News

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, February 23, 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 

 

Goo

 

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 
About Muses Radio Player...
Version 2.1 (html5)

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.
-->

Tangaza nasi

Breaking News
Loading...

Soma App

Soma App
DOWNLOAD Somaapp NOW!

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Monday, April 3, 2017

Day 2: Semina ya Neno la Mungu Dodoma- " Fahamu Ya yafuatayo kuhusu Ndoto unazoota ili ufanikiwe kimaisha" Mwl. Mwakasege

2⃣ *SEMINA YA NENO LA MUNGU  DODOMA UWANJA WA BARAFU*

*NA MWL MWAKASEGE*

*FAHAMU YAFUATAYO KUHUSU NDOTO UNAZOOTA ILI UFANIKIWE KIMAISHA*

*TAR 3 APRIL 2017*

*Siku ya Pili*

LENGO ni kuimarisha mahusiano yako na Mungu katika Kristo Yesu

Kuna mambo 2 ambayo yanaweza kutumika katika NDOTO

*JAMBO 1*
Shetani anaweza kutumia NDOTO kupandikiza mambo ambayo usipoyang'oa mapema yataharibu maisha yako

*JAMBO 2*
Kutazama ishara  zitakazo kuonyesha kuwa NDOTO zinahitaji kufuatiliwa

*ISHARA*
1. Kujisikia kufadhaika moyoni kwa ajili ya NDOTO uliyoota

Kufadhaika  maana yake ni mahangaiko unayoyapata  ndani ya Moyo wako( kuutibua moyo)

_Mwanzoni 41:1-8"...... 8. Hata asubuhi roho yake IKAFAIDHAIKA akapeleka watu kuwaita waganga wote wa misri ..._

⏩Usifanye kosa kudharau NDOTO yoyote utakayoota Ukasema kumbe ni ndoto tu,  inabidi kuifuatilia  _Mwanzo 41. 7 b"Basi Farao akaamka , *kumbe ni NDOTO tu*._

_Mwanzo 40:5-6 "Wakaota ndoto wote wawili, kila mtu ndoto yake usiku mmoja, kila mtu kwa tafsiri ya ndoto yake, mnyweshaji na mwokaji wa mfalme wa Misri waliofungwa gerezani. Yusufu akawajia asubuhi, akawaona *wamefadhaika*._

Yusufu aliwaona wote wawili mnyweshaji na mwokaji wote WAMEFADHAIKA

⏩Mfadhaiko huja kama alarm,maana ukishaitega alarm ikilia lazima ushtuke.

2. Kuota NDOTO hiyo zaidi ya Mara moja au inayofanana na hiyo
⏩Mwanzo 41:25-32
Mst 32"...  _*Na ndoto ya Farao kwa vile ilivyokuja mara mbili, ni kwa sababu neno hilo Mungu amelithibitisha, na Mungu atalitimiza upesi*_.

Unapoota Mara 2 au zaidi ni kukutaarifu unatakiwa kuifuatilia hiyo NDOTO
*Ayubu 33:14-15*
_Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, *Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali*. Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;_

Usipoifuatilia ndipo Mungu huirudisha Mara ya 2 au zaidi hadi utakapopata ufahamu wakulifanyia kazi

⏩Jiulize kama Mungu katumia NDOTO kusema na wewe kwa nini iwe vigumu kuelewa maana yake

_Warumi10:17 Basi imani, chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa *neno la Kristo*._

Ukiwa na Neno LA Mungu lazima utaisikia sauti yake.

⏩Mfano ukiwa na gari ni vema kujua baadhi ya vitu ili likipata shida uweze kulitengeneza sio lazima kila kitu unapeleka garage. Vivyo hivyo kwa watumishi, sio lazima kila tatizo lako unalipeleka kwa watumishi mengine yatatue mwenyewe Yale unayoona huyawezi ndio yapeleke huko, unapotaka kumweleza *Mtumishi jambo lako sikiliza Amani Ya moyo wako kwanza*

3. Ndoto uliyoota kukutia hofu
Daniel 4:5 na Ayubu 4:12-14

_Nikaota ndoto iliyonitia *hofu*; mawazo niliyokuwa nayo kitandani mwangu, na njozi za kichwa changu, zikanifadhaisha._
*DAN. 4:5*

_Basi, nililetewa neno kwa siri, Sikio langu likasikia manong’ono yake. Katika mawazo yaliyotoka katika maono ya usiku, Hapo usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu.  *Hofu* iliniangukia na kutetema, Iliyoitetemesha mifupa yangu yote._
*AYU. 4:12‭-‬14*

4. Ukiwa mambo uliyoota kwenye ndoto yanatokea katika mwili
Ayubu 4:12-16👆👆

Mfano
⏩Ukiona umeota ndoto unakemea na ulivyoshtuka bado unakemea( fuatilia)

⏩Au ulikuwa unalia kwenye ndoto na umeamka unakuta macho yana machozi pia fuatilia

5. Ndoto kukunyima usingizi
Daniel 2:1
 
_Hata katika mwaka wa pili wa kumiliki kwake Nebukadreza, Nebukadreza aliota ndoto; na roho yake ikafadhaika, *usingizi wake ukamwacha*_. *DAN. 2:1*

6. Kwa na hamu ya kutaka kujua tafsiri ya hiyo ndoto
Mwanzo 40:7-8,41:7-8

_Akawauliza hao maakida wa Farao, waliokuwa pamoja naye katika kifungo, nyumbani mwa bwana wake, akisema, Mbona nyuso zenu zimekunjamana leo? Wakamwambia, Tumeota ndoto wala hapana awezaye kuifasiri. Yusufu akawaambia, Kufasiri si kazi ya Mungu? Tafadhalini mniambie.MWA. 40:7‭-‬8 SUV_

_Kisha hayo masuke membamba saba yakayala yale masuke saba makubwa yaliyojaa. Basi Farao akaamka, kumbe! Ni ndoto tu.   Hata asubuhi roho yake ikafadhaika; akapeleka watu kuwaita waganga wote wa Misri, na watu wote wenye hekima walioko. Farao akawahadithia ndoto yake, wala hakuna aliyeweza kumfasiria Farao mambo hayo.MWA. 41:7‭-‬8_

Mstr 8 - alitaka kujua ndoto ile ilimaanisha nini

⏩Ndoto ya Farao ilibeba maisha ya miaka 14 ya dunia nzima,kama angepuuzia sijui ingekuwaje kwa hiyo miaka 14. Kwa hiyo  ule msukumo aliokuwa nao ndio ulisaidia utafsiriwa

7. Ndoto uliyoota kukuletea mahangaiko moyoni mwako juu ya Imani na utumishi ulinao kwa Mungu

_Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu, ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo; wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa BWANA, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda BWANA, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote. Tembeeni kwa kumfuata BWANA, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye.KUM. 13:1‭-‬4_

⏩Usimwogope mtu Bali mwogope Mungu

⏩Usikubali jina au huduma yako ivume kuliko jina la Yesu

*Mfano*: Punda aliembeba Yesu alitembea juu ya nguo kwa sababu tu alikuwa kambeba Yesu lakini baada ya kumshusha Yesu alitembea chini kama kawaida. Dhamani uliyonayo ni kwa sababu unae Yesu ndani yako

8. Ukiona uliyoyaona kwenye ndoto yanapinga au ni tofauti ya mipango uliyonayo

Ayubu 33:14-17
_Kwa kuwa Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara ya pili, ajapokuwa mtu hajali.   Katika ndoto, katika maono ya usiku, Usingizi mzito uwajiliapo watu, Katika usingizi kitandani;  Ndipo huyafunua masikio ya watu, Na kuyatia muhuri mafundisho yao,  Ili amwondoe mtu katika makusudio yake, Na kumfichia mtu kiburi;AYU. 33:14‭-‬17_

⏩unaweza kuota ili upangue kile kibaya ambacho kinaweza kutokea mbele,hivyo anapozungumza nawe anakusaidia usijeingia kwenye matatizo Fulani au kukuondoa katika mawazo uliyonayo

9. Kusikia msukumo moyoni wa kusimulia ndoto uliyoota
Mwanzo 37:5-11( Pale Yusuph alipowasimulia ndugu zake ndoto aliyoota)

Mathayo27:19  _Na alipokuwa ameketi juu ya kiti cha hukumu, mkewe alimpelekea mjumbe, kumwambia, *Usiwe na neno na yule mwenye haki; kwa sababu nimeteswa mengi leo katika ndoto kwa ajili yake*._

⏩Unaweza kuota ndoto kwa ajili ya mtu mwingine hivyo pale unapopata msukumo moyoni wa kumwambia we mweleze ila omba hekima, na kibali kutoka kwa  ROho Mtakatifu

10. Kusikia msukumo moyoni wa kuandika ndoto uliyoota

_Habakuki 2:2-3 BWANA akanijibu, akasema, *Iandike njozi ukaifanye iwe wazi sana katika vibao*, ili aisomaye apate kuisoma kama maji. Maana njozi hii bado ni kwa wakati ulioamriwa, inafanya haraka ili kuufikilia mwisho wake, wala haitasema uongo; ijapokawia, ingojee; kwa kuwa haina budi kuja, haitakawia.HAB. 2:2‭-‬3_

⏩Unaandika kwa sababu unaweza kuisahau asubuhi au kwa  ajili ya kufuatilia huko mbeleni

⏩Uwe unaandika ndoto zakusaidia baadae
Note:Kama huwa unasahau ndoto unazoota weka daftari na kalamu karibu ili unapoota tu uwe unaziandika na baadae iwe rahisi kuzifuatilia hatua kwa hatua.

11. Ukiwa umesahau ndoto uliyoota ila moyoni unajisikia msukumo wa kutaka kujua

Daniel 2:1-5
Baada ya Nebkadreza kusahau ndoto Daniel alienda kumweleza hiyo ndoto tena

⏩Ukiota ukasahau jitahidi kuifuatilia kwani ktk ulimwenngu wa roho imerekodiwa km ile ya Nebukadreza.

MAOMBI
⏩Toba kama kuna mojawapo ya ishara hizi 11 hukuzifuatilia( kwa kujua au kutojua) Mungu arudishe hizo
Ndoto ili aseme nasi tena haijalishi muda gani umepita

🗣🗣🗣🗣🗣🗣🗣
Bwana Yesu Asifiwe. Tunawakaribisha kwenye semina inayoendelea Dodoma mjini katika uwanja wa barafu. Semina imeanza jana tarehe 2 April itaendelea hadi jumapili tarehe 9 April.
Redio zinazorusha Semina inayoendelea Dodoma mjini ni;

1. Redio Sauti ya injili - 
Moshi, 92.2 FM
Arusha,96.1 FM.
Tanga 102.6FM  & 96.7 FM
Same 100.4 FM
Rombo 96.4 FM
Manyara 102.9 FM & 96.1FM
Morogoro 99.1 FM
Mara 96.1 FM
Unguja, Pemba na Mombasa 102.6 FM
Voi - Kenya 96.4 FM
Dodoma 102.9 FM
Pwani, Rufiji, Kiluvya, Tegeta, Ubungo, Manzese, Mbezi, na Ruaha  99.9 FM
Daraja la Mkapa (Lindi) 99.9 FM

2. Redio HHC Alive
Mwanza, Mara, Simiyu, Geita, Kagera, Shinyanga, - 91.9 FM.

3. Redio CG FM
Kigoma, Simiyu, Shinyanga, Tabora na Katavi 89.5 FM

4. Redio Baraka
Iringa, Njombe, Mbeya, Rukwa 107.6 FM

5. Radio Rungwe
Rukwa, Malawi,Mbeya na Njombe102.5 FM

6. Radio Info
Mtwara 92.1 FM

7. Redio Uzima
Dodoma 94.0 FM

8. Redio Bunda FM
Mwanza, Mara, Simiyu na Kagera 92.1 FM

9. Redio Mpanda FM
Katavi, Rukwa na Kigoma 97.0 FM

Unaweza kusikiliza live kupitia www.kicheko.com na www.mwakasege.org, unaweza kusikiliza na kuangalia  live kupitia www.ustream.tv/chanel/mwakasegemanaministry na www.youtube.com (jina la chanel ni Christopher Mwakasege)

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.