Shuhuda za housegirls
Na Apostle Darmacy
Ziko shuhuda nyingi kuhusu House girls au kwa ujumla housemaids
wote-(houseboys, car washers, garden keepers, baby carer, house guards,
cattle keepers, shopkeepers etc. na kila mmoja wetu anaweza kua na
experience nao tofauti, kati ya hizo, nyingine chungu sana. Mara nyingi
wengi wetu tunasimulia negative tu kuhusu wasaidizi hawa wa nyumbani na
kwakweli ni somehow fair kwa kuwa ndio hayo mabaya tuliyokumbana nayo
au waliotufanyia Ni kusudi la shuhuda hizi zifuatazo, tugeuzwe
mitazamo/nafsi zetu na namna tunavyowa-treat ili kabla ya kuwatimua
(when it is only the critical alternative), tupate nafasi kidogo ya
rehema, kujaribu kutumia hatua za kiroho badala ya zile za kimwili(
ukali, kupiga fimbo, zaba vibao vya hatari, kukata au kufuta mshahara,
e.g. kwa kuwa amevunja chupa ya chai, kufoka, tukana, hata wengine kutia
ndani kituo cha police.
Shuhuda No. 1:
Mdada anaishi Pugu, ameokoka, ana mume na watoto. Alipata housegirl toka
Mkoa wa Iringa, msichana yatima, umri wake miaka 16, aliyelelewa na
Bibi na Babu. Katika ukoo wa huyo housegirl, ni watu wa mizimu na uchawi
kemkem na ni kawaida kurithisha ‘hazina’ yao hiyo kizazi kimoja kwenda
kingine. Msichana huyu alifanyiwa urithishaji huo akiwa mdogo zaidi na
hata kufikia hatua nzito za kichawi za ku-operate mambo makubwa ya
kuzimu. Hatimaye alivikwa pete maalumu baada ya kufuzu mambo mazito ya
'devo' (shetani) na kuwa malkia wa wachawi kwa anga la upande ule wa
eneo lao.
Katika kutafuta msichana wa kazi, Mpendwa huyu wa Pugu akawa amempata
binti huyo mwanga na yatima. Akawa anafanya kazi kama kawaida na
anafundishwa vitu vipya vya ki-Dar kama vifaa vya upishi na mengine,
akawa anaelewa na maisha yakaendelea vema. Kitu kimoja kikawa
kinamshangaza mpendwa ni kwa nini mtoto kama huyo awe na pete mithili ya
ile ya ndoa na kamwe hasingeivua ktk mazingira yoyote! Hata kila
alipoulizwa na bosi wake, kwanini ana pete ya ndoa na umri wake mdogo,
je ameolewa au kuposwa kimila? Alikaa kimya tu na hakuwahi kutoboa siri.
Siku zikaeendelea, kazi anafanya, tabia yake njema kabisa, adabu tele
lakini kila mara mpendwa akiona ile pete na kulinganisha na umri wake,
inamsumbua kweli. Akaamua kufunga na kuomba na kisha akahakikisha kila
ibada za nyumbani jioni, house girl hafanyi kazi nyingine, shurti
ashiriki ibada pia. Siku zikapita mpendwa akaamua kuacha ubosi na
kutafuta/kujenga urafiki sana na taratibu kwa mapenzi akawa anamuuliza
kuhusu ile pete. Kwa namna vile bosi wake alivyomchukua kama rafiki e.g.
wanapiga story na kucheka, kufurahi, si Housegirl akafunguka! Akaweka
yote hadharani! kumbe ile pete ilikua ni mhuri wakiapo cha kufa cha
nguvu za ajabu katika ulimwengu wa roho wa giza na alama ya mamlaka ya
utawala aliokua amevikwa kuwa juu ya wachawi kwakuwa pia alikuwa mshauri
wao (resourceful person/technical expert if you
like).
Ndipo mpendwa akamhubiria kirafiki kweli na kumhakikishia akikubali
kuvua na kumkaribisha Yesu ndani, hatakufa kama alivyoambiwa katika
viapo na kafara. Katika ibada moja, wakafanya maombi kisha kuanza
kuivua, walipokua wanaitoa, ghafla instinctively, vidole vya binti
vikajikunja kwa nguvu ya ajabu, walifanya mechanical efforts kuvifungua
ikashindikana. Kisha wakaliitia jina la Mfalme juu ya Wafalme na kuamuru
violently mashetani yaachie vidole vile, ghafla vikanyooka kisha
wakaivua. Ilipotoka tu, akaanguka chini kisha madude kuanza kelele,
wakakemea na binti akawa sawa. Walipoamka kesho yake, to their surprise,
pete ilikua imerudikwa kidole ila ya aina nyingine kama
cheni/kambakamba ivi. Wapendwa wakaweka gear kubwa zaidi ya maombi ndipo
hatimaye wakaitoa ile pete-kamba.
Walipolala binti anasema waganga wa kienyeji 8 wa Dar es Salaam ambao
walikua wanapata ushauri kwakwe akiwa Iringa, walimjia usiku, yeye binti
anawaona kabisa but wapendwa hawawaoni. Halafu ile pete ya pili
ilipotoka, mpendwa akapata simu toka kwao binti kuwa kwa nini wamemvua
pete ya ukoo! Mpendwa alishangaa kweli, wamejuaje?! Baada ya siku,
ukatumwa ujumbe kuwa ukoo wanamtaka mtoto wao arudishwe nyumbani mara
moja. Mpendwa akawa katika dilema, housegirl si mtoto wake wa kuzaa but
ni mwanae kiroho kwa kuwa siku zilizofuata, aliamua kuokoka kabisa baada
ya maombi mengi ya kumweka huru, na hapo hapo Ukoo unamdai mwana wao,
je amwachie aende na uchanga ule kiroho au awakatalie wenye haki yao?
Akafanya maamuzi magumu lakini ya imani, akamruhusu kwenda home baada ya
kumwombea/kumzidika kiroho kisha kumuelekeza atajibu nini na
kumsisitizia kusimama kwa dhati na Yesu ikibidi kufa ili aende mbinguni.
Akafika home, kikao kikubwa cha ukoo, wakamweka kati, wakimtishia
kumlaani, na kua atakufa/mizimu itamyonga na mambo mengi ila akivishwa
tena pete ya urithi, yote hayata mtokea. Binti alisema statement hii
mbele ya Wazee, Mashangazi na waganga wa ukoo…
"MIMI NIMEAMUA KUMPOKEA YESU NA KUOKOKA NA SITAVAA TENA PETE
YOYOTE KUBEBA URITHI HUU WA KICHAWI WA UKOO MPAKA NITAKAPO VALISHWA PETE
KANISANI NA MUME WANGU".
Baada ya kujibu ‘kijeuri’ hivyo, walimkamata kwa nguvu na kuanza
kumvisha. Kelele na kilio kilisikika nyumba za jirani na kumbe mojawapo
ya majirani ni mchungaji aliyeokoka. Akachukua baadhi ya watu na kwenda
hapo. Kuuliza kulikoni, yule Housegirl, akapayuka walichokua wanataka
kumfanyia..Ndipo Mchungaji akawasihi wasifanye ivyo, ni kufuru kwa
Mungu. Mchungaji akawaambia angependa kuongea na Wana ukoo jambo la
muhimu hivyo atawatembelea, kesho yake ilikuwa pasaka.
Mchungaji hakufanya kosa na hatimaye, UKOO MZIMA SIKU ILE WALIAMUA
KUOKOKA. Kupitia mpendwa aliyemchukulia housegirl kwa moyo wa kitumishi,
wokovu ukaingia kwa binti huyo na hatimaye kupitia kamdada hako, ukoo
wake wa wachawi, sasa ni wana wa Mungu na mashahidi wa imani ya kweli ya
kuokoka ibadilishayo maisha ya mwanadamu wa aina yoyote.
Shuhuda No.2:
Mdogo wangu anaishi Mtwara na mkewe. Walipata mtoto na baada ya muda,
akaanza kuugua malaria kila mara. Wakatumia njia zote kumtibu, namely
vidonge, sindano na kisha drips, anapona lakini baada ya wiki, anaugua
tena, ni malaria tu mwanzo mwisho. Ikawa ni mateso na huzuni kwa mkewe
na huruma kweli kwa maana mtoto mdogo kudungwa sindano kila mara, ilikua
ni sikitiko kweli katika nafsi za wazazi.
Ikatokea siku moja tafakari ikamjia mkewe kuwaza sana nini hasa chanzo
cha mateso/malaria isiyoisha kwa kipenzi mwanae wakati wanapiga dawa na
kutumia net? ghafla moyo wake ukamuelekeza kufikiri sana kuhusu
housegirl aliyekua naye. House girl wake ingawa alikuwa ni mdogo lakini
alikuwa mkorofi kweli, kiburi pia kikatili, kitafanya kazi vema
kitakapojisikia, ukikirarua/fokea tu, kinavimba, mbinde haswa mpaka
uli-reconcile diplomatically ili ku-win her cooperation katika kazi
nyingi home pale.
Siku moja shemeji akaamua kumhoji kirafiki ili kumfahamu kwa undani.
Ndipo binti yule wa umri wa miaka 15 akawa wazi na akasema, Bibi yake
huwa anamfuata na wachawi wenziwe kila usiku wanamchukua yeye na mtoto
wa shemeji yangu kwenda kutambaa uko ulimwenguni katika roho na
kumrudisha saa kumi na moja asubuhi. Shemeji hakujua kumbe alikua
analala na ‘mtoto-ritufe’ na kuwa pale kitandani kwa binti wa kazi,
alikua ni ‘ridude-housegirl’. Kikaongea mengi kuhusu waliyokuwa
wanamtenda mtoto wake mpaka shemeji alipata pressure jioni hiyo hiyo
kwakuwa hakuamini kuwa mtoto wake mpenzi kifungua mimba, alikua
anatwaliwa/ kupaishwa kwenda katika mikutano, ibadani, mazindikoni na
makazi ya wachawi na kuwa kitandani alikua analala na kunyonywa na
‘ritufe mtoto’!!.
Walifanya maamuzi ya kutomtimua housegirl kurudi kwao kijijini but
kumpeleka kanisani akaombewe. Wakati wa maombi, mtoto wa shem alikua
anageuka-geuka/jinyonga-nyonga kama nyoka na pia housegirl kama mnyama
akitoa sauti kama simba dume. Walifanya maombi ya deliverance kwa masaa
ndipo wote wakapona kabisa na kufunguliwa moja kwa moja. Walipomuuliza
binti kama angependa kumpokea Yeye aliyemfungua, akakubali kwa machozi,
wakamuombea kuokoka. Tokea hapo, ukawa mwisho wa malaria isiyokwisha na
‘trips’ za usiku ulimwenguni uko. Tendo hilo lilimfanya shemeji na mdogo
wangu kuamua kwa dhati sasa kuokoka maana walikua ni watu tu wakwenda
kanisani, wanakubali kila kitu yet hawafanyi rocket decision to confess
Jesus. Thus, kupitia house girl mwanga, wokovu ukaingia kwake,
kakang’olewa toka nguvu za giza hatari na hatimaye pia shemeji na dogo
leo ni indeed Biblical Pentecostal born again.
I wanna challenge you all in Jesus name, tuangalie/ku-revist namna
tunavyoishi nao, je tunawa-treat vipi?- kama dogs, empty bottles of
Kilimanjaro water or human beings? je tunawachukulia kama nao pia ni
target ya moyo wa Yesu kufa msalabani in case hawajaokoka hivyo kukaa
nao ki-mkakati injili? Je tuna rehema yoyote ya kujaribu kuona tabia
walizo nazo, nyingine zitakua ni manifestations za mambo waliyofanyiwa
at their tender age? Je kwa upendo wa calvary au kibinadamu/kiutu tu,
unawatengenezeaje future housemaids wako kama wanakuja kwako labda
hawajui kusoma na kundika Kiswahili-hawakwenda skuli kabisa,hawajasoma
English kozi kidogo, wengine wameishia darasa la 7, kidato cha 4, 6? Je
kweli roho na nafsi yako kama uliyeokoka vinakupa raha kuwatumia tu
miaka 2, 3,6,10 wakiwa wamebaki tu hivyo? Hata mafunzo ya ususi wa
nywele za kimasai, saloon, cherehani huna mpango? Unasimamaje
kuomba/ku-preach/teach mbele za Bwana na watu with such devilish black
spot ya kuwa ‘the master of home/domestic neo-colonialism’? Can you
imagine? 2, 3, 4, 6, 10 years bila kumuendeleza lakini unamkamua jasho
toka sa 11 asubuhi hadi saa 5 usiku kila siku na mshahara ule ule wa
alfu 6, 10, 15, 20 kwa life ya leo hii!? yet confidently in the
church/altar, una-'shandabaraise!!'… ni dhambi mbaya( dhuluma).
Press on revisiting our relationships, handling and perceptions kama mabosi towards our housemaids, notably house girls.
Toa Maoni Hapa Chini