Msiba wa Baba
mzazi wa Mwimbaji gospel nchini Bahati Bukuku
Hizi ni baadhi ya picha za msiba wa baba
mzazi wa mwimbaji gospel nchini Bahati Bukuku aitwaye mzee Lwaga Bukuku
ambaye alifariki dunia hivi majuzi jijini Dar es salaam. ambapo msiba
ulikuwa nyumbani kwa mwimbaji huyo maeneo ya Tabata, watu mbalimbali
wakiwemo waimbaji wenzake Bahati kama David Robert, Jennifer Mgendi,
Christina Shusho,Jane Misso, Christina Matai, Neema Gasper na wengine
walifika nyumbani hapo kumpa pole, mwili umesafirishwa kuelekea mkoani
Mbeya kwa mazishi.
 |
| Nyumbani kwa Bahati |
 |
| Christina Matai. |
 |
| Watu wakiwa msibani. |
 |
| Jane Misso akimsifu Mungu. |
 |
| Watu wakitoa heshima za mwisho. |
 |
| Msiba nyumbani kwa Bahati. |
 |
| Bahati akiwa na wafiwa wengine. |
 |
| Wafiwa wakipata chakula kabla ya ibada ya mazishi kuanza. |
 |
| Baadhi ya waimbaji wakiongozwa na Christina Shusho wakiwa msibani hapo. |
 |
| Neema Gasper akimsifu Mungu huku akipewa nguvu na mwana GK Silas Mbise. |
 |
| Silas Mbise akilonga huku Joshua Makondeko akifurahia maneno ya busara kutoka kwa kijana. |
 |
| Chakula kilihudumiwa na kampuni ya Bahati inayojihusisha na mambo ya vyakula. |
 |
| Bahati akizungumza jambo. |
 |
| Solomon Mukubwa akiimba msibani hapo. |
 |
| Beatrice Mwaipaja akiimba. |
 |
| Jeneza lenye mwili wa marehemu mzee Lwaga Bukuku. |
 |
| Mchungaji akiongoza ibada ya mazishi. |
 |
Bahati Bukuku akiwa na wafiwa wengine wakati wa ibada ya kuuaga mwili.
Hata hivyo alamanusura mambo yaende
kombo, ambapo utata ulijitokeza wapi mwili uzikwe, kati ya Mbeya ama
jijini Dar eneo la Sinza, ambapo kaburi lilichakuwa limeandaliwa,
tofauti na mipango mingine ilivyokuwa.
Tukio hilo ambalo limeshuhudiwa , lilianza
kufukuta pale ambapo ilitangazwa kuwa marehemu Lwaga Bukuku angezikwa Mbeya,
jambo ambalo lilizua taharuki kwa baadhi ya wafiwa ikiwemo watoto, ambapo
baadhi waligoma kuaga mwili – huku kaburi lililokuwa limeandaliwa maeneo ya
Sinza, likibaki tupu bila kujua nini kinafuata.
BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIBARIKIWE.
Picha Ni kwa hisani ya http://gospelkitaa.blogspot.com
| | | | | | |
Toa Maoni Hapa Chini