NI MOJA YA MIKUTANO YA NENO LA MUNGU JIJINI- MBEYA 2013
Mkutano
wa Injili wa neno la Mungu katika kanisa la T.A.G Forest karibu na
mahakama kuu ya jijini Mbeya Ulianda mkutano mkubwa wa neno la
Mungu ni katika viwanja vya kanisa mwaka 2013 ambapo mkutano ulihudumiwa na
Mchungaji Chistopher kutoka Morogoro
 |
Mchungaji Chistopher,Mchungaji msaidizi Thobias Tambikeni na Mzee wa kanisa Dr.Nehman
|
Somo la siku ya leo lilitoka katika kitabu cha Matendo ya Mitume 4;1 ambapo biblia inasema "
hata walipokuwa wakisema na watu wale,Mahuhani na Akida wa hekalu na
masudukayo wakawatokea wakifadhaikka sana kwa sababu wanafundisha watu
kuhubiri katika Yesu ufufuo wa wafu.
Wakawakamata
,wakawaweka gerezani hata asubuhi kwa kuwa ilikuwa jioni. Lakini wengi
katika hao waliosikia lile neno waliamini,na hesabu ya watu waume ikawa
kama elfu tano.
walipo waweka katikati wakawauliza kwa nguvu gani na kwa jina gani ninyi mmefanya haya ?
Ndipo
petro ,akijaa Roho Mtakatifu, akawambia, Enyi wakubwa wa watu na wazee
wa Israeli, Kama tukiulizwa leo habari ya jambo jema alilofanyiwa yule
mtu dhaifu ,jinsi alivyoponywa, jueni ninyi nyote na watu wote wa
Israeli ya kuwa Kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti ambaye ninyi
mlimsulubisha, na Mungu akamfufua katika wafu
Kwa
jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu . Yeye ndiye jiwe
lile liliodharauliwa na nyinyi waashi nalo limewekwa kuwa jiwe kuu la
pembeni .
Wala
hakuna wokovu katika mwingine awaye yote ,kwa maana hapana jina jingine
chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupaslo sisi kuokolewa kwao.
Mchungaji Chirstopher alisimama na kuanza kuhubiri kwa kusema leo jion yenye matarajio makubwa maana Mungu wetu humuinua mnyonge kutoka mavumbini na kumketisha juu na wakuu na wafalme wa nchi.
Bwana Yesu alikuja duniani ili kuukomboa ulimwengu kutoka kwenye dhambi.
JE? ni nini kinacho kutesa sasa shida muda mrefu ,magojwa yasiyo pona ,fedha hali ngumu ya uchumi,ndoa ina migogoro Nasema leo leo Yesu mtenda miujiza yuko hapa kukuhudumia.
Petro alijibu vema kwa kusema "Enyi
wakubwa wa watu na wazee wa Israeli, Kama tukiulizwa leo habari ya
jambo jema alilofanyiwa yule mtu dhaifu ,jinsi alivyoponywa, jueni ninyi
nyote na watu wote wa Israeli ya kuwa Kwa jina la Yesu Kristo wa
Nazareti ambaye ninyi mlimsulubisha, na Mungu akamfufua katika wafu"
Yeye ndiye jiwe lile liliodharauliwa na nyinyi waashi nalo limewekwa kuwa jiwe kuu la pembeni .
Wala
hakuna wokovu katika mwingine awaye yote ,kwa maana hapana jina jingine
chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupaslo sisi kuokolewa kwao.
Aidha Mchungaji Chirstopher alisema yeye akushawishi wewe kuokoka bali wewe binafsi ndio unatakiwa kushawashika
na kumpokea Kristo kuwa Bwana na mWokozi wa maisha yako maana watu
maelfu wanamkimbilia yeye ambaye ni Tabibu wa kweli.
Pia alisema sasa si wakati wa kushabikia dini, Bali ni kutangaza kazi ya msalaba wa Bwana Yesu Duniani kote maana ni agizo kutoka kwa Bwana.
Kitendo cha kina Petro kwenda gerezani watu waume elfu tano waliweza kuokoka. Pia alisisitiza kwa kusema hata kwa kupigwa kudhralailiwa na kukejeliwa mimi nitatangaza injili ya Bwana Yesu aliye hai.
Katika gerereza Kina Petro walifanya maombi, walifanya mlima wa maombi wakati wapo gerezani.
Na walipo pelekwa katika baraza waliulizwa " kwa nguvu gani na kwa jina gani ninyi mmefanya haya ? Kwa maana nyingine nao walitaka kujua siri iliyopo ndani ya Yesu tunaye muhubiri leo. Petro akiwa amejaa Roho alijibu na kusema "
Enyi wakubwa wa watu na wazee wa Israeli, Kama tukiulizwa leo habari ya
jambo jema alilofanyiwa yule mtu dhaifu ,jinsi alivyoponywa, jueni
ninyi nyote na watu wote wa Israeli ya kuwa Kwa jina la Yesu Kristo wa
Nazareti ambaye ninyi mlimsulubisha, na Mungu akamfufua katika wafu
Kwa
jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu . Yeye ndiye jiwe
lile liliodharauliwa na nyinyi waashi nalo limewekwa kuwa jiwe kuu la
pembeni .
Wala
hakuna wokovu katika mwingine awaye yote ,kwa maana hapana jina jingine
chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupaslo sisi kuokolewa kwao.
Ukiwa na Jina la Yesu ndoa yako itakuwa salama,maisha yako yatakuwa salama,pia utapata mambo mapya na makubwa maana Bwana ni mwaninifu kwa watu wake.
Hata kama huna pesa, umekosa ada ya shule ,huna kazi mtegemee Bwana Yesu maana yeye ndiye mwenye hazina iliyo kuu pia kumcha Bwana ndio chanzo cha Maarifa.
KWA NINI TUNA MUHUBIRI MUNGU
NI agizo; Mathayo 28;19 inasema " Basi Enendeni
mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi mkiwabatiza kwa jina la baba na
mwana na Roho mtakatifu na kuwakundisha kuyashika yote niliyo wamuru
ninyi, na tazama mimi niko pamoja nanyi siku zote hata ukamilifu wa dahari
Watu wamepotea katika Dhambi; Warumi
6;23" Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni
uzima wa milele katika uzima wa milele katika kristo yesu Bwana Yesu
Bwana wetu"
Dhambi ni mbaya sana ina uwa,inaleta majuto, imefanya watu kuwa na hali mbaya achana na tamaa mbaya ili dhambi iondolewe ni kwa umkiri bwana yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa Maisha yako.
Pia Alitoa shuhuda juu ya maisha yake ambapo alisema wakati yuko mdogo walikuwa wanaishi Singida Walikuwa wanaishi katika gunia la kutokuwa na matumaini. Alisema "kulikuwa na bibi mmjo hapo kijijini kwa alikuwa ni mchawi sana iyo siku nikamkanyaga kwa bahati mbaya mtoto wa yule bibi na akaanza kulia huku akienda kwao nilijaribu kumembeleza lakini hakunisikiliza na alikwenda kwa bibi yake na kumwambia;
Kilichotokea majira ya saa nane usiku nilianza kuchapwa viboko na sion mtu anaye nichapa.Asubuhi mama alinipeleka kwa mganga na tukapewa dawa. Ki ukweli baba alikuwa ni mlevi ivyo alikuwa anarudi usiku sana . ilipofika asubui mama alimweleza juu ya hali yangu na hapo alikuja na kunitazama nami nikamsimulia yote,
Hapo hapo baba akachukua Panga na kwenda kwa yule bibi na alipofika akamwambia Mwanangu akifa ama zangu ama zako nitahakikisha nawe unakufa akatoa panga na kulinoa jiwe"
Licha ya yule bibi kuwa mchawi lakini aliogopa hapo tunjifunza kuwa wachawi ni waoga hawana kitu pia wanaogopa kufa maana wanajua wanakoenda ni jehanamu kwenya moto wa umilele. lakini watu wa Mungu wanatumaini la kuishi na Bwana Yesu Mbinguni.
FANYA UAMUZI SASA KWA KUMKILI BWANA YESU KUWA BWANA NA MWOKOZI WA MAISHA YAKO MAANA HUKO NDIKO KUNA USALAMA.
 |
Na Mwandishi wetu Damacy
|
Toa Maoni Hapa Chini