MUNGU WETU NI MUNGU WA KUHESHIMIWA
Hawa ni baadhi ya watu maarufu duniani waliomdhiaki Mungu na kupata adhabu.
1. JOHN LENNON (MUIMBAJI)


Wakati alipokuwa akihojiwa na mwandishi wa habari wa gazeti la American
alinukuliwa akisema hivi "Ukristo utakufa na kutoweka duniani, siwezi
kuwa na wasiwasi na hilo kwa kuwa nina uhakika nalo. Mafundisho ya Yesu
yalikuwa sahihi na wala sipingi hilo ila mafundisho yale yalikuwa mepesi
sana ambayo mtu yeyote anaweza kuyafundisha. Hebu angalia leo, tumekuwa
maarufu hata zaidi yake (Hapo alilitaja kundi lake la The Bettle).
Ilikuwa mwaka 1966.
Wiki moja baada ya kutamba kwamba yeye na kundi lake lilikuwa maarufu hata zaidi ya Yesu, akapigwa risasi sita na kufariki.
2. TANCREDO NEVES (RAIS WA BRAZIL)

Alisema kwamba endapo angepata kura laki tano kutoka katika uchaguzi
mkuu wa Brazil na kuwa rais, hata MUNGU asingeweza kumtoa katika urais
huo. Akafanikiwa, akapata kura zaidi ya hizo, akashinda uchaguzi, siku
moja kabla ya kuapishwa, akafariki dunia.
3. CAZUZA (MWANAMUZIKI WA BRAZIL)

Alipokuwa katika shoo yake ndani ya jiji la Rio De Janeiro, alichukua
sigara, akaanza kuivuta, akachukua nyingine na kisha kuirusha juu na
kusema "Mungu, hiyo yako, chukua nawe uvute"
Alifariki akiwa na miaka 32 kwa ugonjwa wa kansa ya mapafu ambayo iliyaharibu sana mapafu yake kuliko mgonjwa yeyote yule.
4. MTENGENEZAJI WA MELI YA TITANIC.
Baada ya kutengeneza meli ya Titanic, mwanahabari akamuuliza ni kwa
kiasi gani ilikuwa salama nae akajibu "Ni salama sana, haiwezi kuzama na
hata Mungu hawezi kuizamisha"
Nafikiri unajua kilichotokea kuhusu Titanic.
5. BON SCOTT (MUIMBAJI)
Mwimbaji huyu ambaye alitamba miaka ya 70 alitoa wimbo wake mmoja mwaka 1979 wenye maneno haya
"Don't stop me; I'm going down all the way, down the highway to hell'.
Tarehe 19 February mwaka 1980, alikutwa amekufa baada ya kupaliwa na matapishi yake.
6. Mwanamke mmoja alikuwa akihofia sana kuhusu ulevi wa marafiki wa
mtoto wake. Wakati wanataka kuondoka na gari, akamshika mtoto wake mkono
garini na kumwambia "Binti yangu, Mungu awatangulie katika safari yenu"
Yule binti akajibu "Gari imejaa mama, huyo Mungu labda akae kwenye
boneti la gari".
Baada ya masafa fulani ya safari yao, gari lile
lilipata ajali kiasi ambacho hata polisi hawakujua ni aina gani ya gari
lilikuwa. Lilikuwa limebondeka sana na watu wote walikutwa wamekufa.
Kilichowashangaza polisi, trey la mayai wala halikuonekana kuguswa na
hakuna hata yai moja lililokuwa limevunjika na wakati gari lilibondeka
mpaka kutokutambulika.
7. CHRISTINA HEWITT (MWANDISHI WA HABARI)
Huyu alikaririwa akisema hivi "Nimesoma vitabu vyote duniani, ila hakuna kitabu kibaya...kibaya na kibaya kama Biblia"
Siku chache baada ya kusema maneno hayo, mwili wake ulikutwa umeunguzwa
na moto ambao haikujulikana mpaka leo ule moto ulisababishwa na nini.
8. MARILYN MONROE (MUIGIZAJI)
Huyu alifuatwa na Bill Graham na kumwambia kwamba alitumwa na Roho wa
Mungu kwa ajili ya kumhubiria. Alimkaribisha ndani, akamsikiliza kwa
makini, alipomaliza akasema "Simhitaji Yesu wako, unaweza kuondoka nae".
Wiki moja baadae, alikutwa amekufa katika makazi yake. Polisi
walijaribu kuchunguza kipi kilimuua, mpaka leo hawajapata jibu.
Kwa wale wanaotaka kujua mengi, wafungue GOOGLE na kisha kusearch haya "People who mocked GOD and died" Utasoma mengi tu


Toa Maoni Hapa Chini