MKUU WA WILAYA YA IRINGA AONGOZA CHANGIZO LA KWAYA KUU KANISA LA KILUTHELI KIHESA NA KUFANIKIWA KUPATA MILLION 8,950,000 | Apostle Darmacy Blog MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 | Apostle Darmacy Blog

APOSTLE DAMAS

Breaking News

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, February 23, 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 

 

Goo

 

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 
About Muses Radio Player...
Version 2.1 (html5)

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.
-->

Tangaza nasi

Breaking News
Loading...

Soma App

Soma App
DOWNLOAD Somaapp NOW!

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Sunday, June 12, 2016

MKUU WA WILAYA YA IRINGA AONGOZA CHANGIZO LA KWAYA KUU KANISA LA KILUTHELI KIHESA NA KUFANIKIWA KUPATA MILLION 8,950,000



Mhe Richard Kasesela mkuu wa Iringa mjini Leo alikuwa mgeni Rasmi katika changizo la kwaya kuu ya kanisa la Lutheran Kihesa  Iringa.
Ambapo katika changizo hilo  watu mbalimbali walishiriki baadhi yao ni pamoja na
Askofu Mkuu wa Wa Kanisa la Kilutheri  Dayosisi ya Iringa  Dr. O.  Mdegela pamoja na Makamu mkuu wa Chuo Kikuu Iringa Prf. Joshua Madumulla pamoja na wengine wengi wakiwemo Wachungaji, viongozi wa serikali pamoja na washirika.
Lengo la changizo hilo ni kutaka kufanya Ununuzi wa mashamba ya Miti
Kurekodi video na Audio ya Kwaya Kuu 
Pia kuanza kutoa Huduma za jamii mfano kuona wangonjwa, kusaidia yatima pamoja na watu wenye mahitaji mbalimbali

Pia Mkuu wa Wilaya Mhe Richard Kasesela amesema amehaidi kutoa   shilingi laki tano na kwa kwa ajuli ya changizo ilo. sambamba na hayo changizo hilo ilipatikana takribani  Millioni nane laki Tisa na hamsini 8,950,000/=Tsh

Kumtolea Mungu Fedha na Mali.

Eneo jingine lililo la muhimu sana katika maisha ya mwamini ni eneo la utoaji wa fedha na mali kwa ajili ya Bwana. Eneo hili ni muhimu sana kwa kuwa ni sababu kubwa sana ya Mungu kubariki watu wake na kwa mtu ambaye amekosa uaminifu katika hili eneo ukaaa chini ya laana ila kwa aliye mwaminifu uwa ndani ya Baraka.
Kuna aina mbali mbali za utoaji wa fedha na mali, aina hizo ni kama:

A.     Sadaka ya kuwasaidia watu walio katika uhitaji.
Hii ni sadaka ya mtu kumsaidia mtu haswa Yule ambaye hana matumaini na hana msaada kwa kutoa vile alivyonavyo na kumpatia. Hii ni sadaka ya upendo kwa kuonyesha kumpenda Mungu na kumpenda Yule unayemsaidia.

Hii ni sadaka ambayo mtu anaifanya mbele za mtu kwa ajili ya Mungu, na ikifanyika kwa mtu kujitakia utukufu wake huwa haina thawabu mbele za Mungu ila ikifanyika kwa moyo wa kupenda na kumtukuza Mungu ni njema na ubeba thawabu kubwa mbele za Mungu.

Luka 6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa kifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakacho pimiwa.”  Yesu anapotoa neno hili anazungumza na watu walioamini kuwa imewapasa kutoa vitu vyao kwa watu(wenye uhitaji) ila kutoa kwao si bure kwa kuwa ni lazima Mungu atawarudishia tena  kupitia watu,  si kama walivyotoa bali ni zaidi kwa kipimo cha kujaa  na kushindiliwa na kusukwa-sukwa hata kumwagika.

Mfano wa sadaka hii katika biblia ni:
       Sadaka ya Rahabu kujitoa na kujihatarisha ili wapelelezi kutoka Israeli wapone.
Kitabu cha Yoshua 2:1-6
       Sadaka ya BWANA Yesu kwetu wanadamu.
Kitabu cha Isaya 53
       Sadaka ya mjane wa Sarepta kwa Eliya.
Kitabu cha 1 Wafalme 17:13-16 “
       Sadaka ya Kornelio kwa watu wenye shida mbali.
Kornelio alikuwa mtoaji sana na aliwapa watu sadaka nyingi sana, kama inenavyo katika Matendo ya mitume 10:2 “mtu mtauwa, mchaji wa Mungu, yeye na nyumba yake yote, naye alikuwa akiwapa watu sadaka nyingi, na kumwomba Mungu daima.
Sadaka ya mtu kujitoa na kutoa vitu vyake vya thamani ni sadaka yenye thamani sana mbele za Mungu na ni ishara ya kuwa mtu anampenda Mungu na yule anayemsaidia.

B.     Sadaka kwa ajili ya kuendeleza kazi ya Mungu.
Sadaka hii huitwa kwa majina mengi, na wengine huiita sadaka ya lazima. Wengine matoleo, wengine upenda kuiita sadaka ya ibada. Hii sadaka utolewa kila watu wa Mungu wakutanikapo pamoja kufanya ibada, na mlengo mkuu wa sadaka hii ni kuiendeleza kazi ya injili ipate kusonga mbele.

Ni sadaka ambayo utumika kuimalisha miundombinu ya kanisa, na pia kuwa saidia watumishi wa Mungu, na shughuli nyingine nyingi kama ilivyopangwa na kanisa husika la mahali pamoja. Hii ni sadaka muhimu sana na ni ya lazima kwa kila muumini kuangalia kuitoa kila anapokuwepo ibadani.
Hii ndiyo sadaka inenewayo kuwa usiingie nyumbani kwa BWANA mikono mitupu.

C.     Sadaka ya malimbuko.
Hii ni sadaka ambayo ni ya mwanzo wa kila pato ulipatalo katika yale uyafanyayo. Kama ni biashara basi yale mapato ya kwanza ni malimbuko yako kwa BWANA, kama ni kazi huwa mshahara wa kwanza, kama ni mazao uwa yale ya kwanza na vivyo hivyo kwa wanyama. Sadaka hii pia kwa nyakati za leo uwasilishwa kanisani.

D.    Sadaka ya shukrani
Kitabu cha Zaburi 50:14
Hii ufanywa kwa lengo la kumshukuru Mungu kwa lile lililotokea katika maisha liwe zuri au baya.
Mwalimu Mwakasege anaielezea kuwa ni sadaka ya muhimu kuifanya kila wakati unapofanyiwa jambo au unapokumbwa na jambo, na uelezea kuwa hii ni sadaka ya msingi sana kumshawishi Mungu azidishe utendaji wake katika maisha ya mwamini.

E.     Nadhiri.
 Zaburi 50:5
Matendo ya Mitume 5:1-11

F.     Fungu la kumi.
Malaki 3:8-12
Hii ni sehemu ya kumi ya mapato yako yote uyapatayo, ni  sadaka muhimu sana ambayo pia ipo kwa ajili ya kuiendeleza kazi yake.


Halleluya Sifa na Utukufu nui Kwa Bwana Yesu!!!
TAZAMA BAADHI YA PICHA KATIKA CHANGIZO HILO

























COHELA MEDIA PRODUCTION KATIKA LIVE VIDEO PAMOJA NA PICHA ZA MNATO

MR. MSIGALA KUTOKA COHELA MEDIA PRODUCTION KATIKA LIVE VIDEO PAMOJA NA PICHA ZA MNATO









Anthony Damas Blogger
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.