Thursday, February 23, 2017
MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017
- Next You are viewing Most Recent Post
- Previous Denice Simeo Youth Development Expert atoa ushauri kwa vijana wa chuo
google+
There is greatness inside of you
I believe that there is a seed of greatness in all human beings. Therefore the aim of my blog is to bring to my readers awareness of things that are happening around us. I will focus majorly on inspirational news that can motivate my readers to doing more with their lives too. If you are too busy to get acquainted with what is in the newspapers or you have read the papers but have not felt any inspiration or motivation, please log on this page and be inspired to walk in your purpose and dream.
✨💧💐🌷💫🌱🙏🏻✨💧💐🌷💫🌱🙏🏻🌴✨💧💐🌷
SEMINA YA NENO LA MUNGU
MWL: CHRISTOPHER MWAKASEGE
SOMO: NAMNA YA KUOMBEA NDOTO ZILIZOGUSA MAISHA YAKO
ENEO: MBEYA
SIKU : 4
TAREHE: 13th OCT 2016
💝LENGO LA SOMO:
Kuimarisha Uhusino Wako Na Mungu Katika Kristo Yesu
✳-JAMBO LA NNE LA KUZINGATIA.-
Kuombea tafsiri ya ndoto husika kusikusahaurishe kuombea Ujumbe ulio bebe ndoto hiyo.
🔆Mambo Matatu ya kukumbuka🔆
1⃣: Lengo la kuletewa ndoto ni kuletewa ujumbe.
Ayubu 33:14-15
✅Mungu anatumia njia moja wapo ya ndoto kusema na mtu au watu kutelemsha ujumbe
🔴Pia fahamu. Hata kama chanzo cha ndoto sio Mungu, Mungu bado anaweza kutumia hiyo ndoto kukusaidia kwa kutumia ujumbe wa ndoto hiyo hiyo.
Torati 13:1-4
❇UKIFATILIA NDOTO VIZURI UTAGUNDUA VITU VIFWATAVYO❇
1: Kuna ndoto zilizo beba vitu vinavyoitaji tafsiri ili upate ujumbe ndani yake.
Mwanzo 40:5-23
✅Kuna ndoto zinavitu ndani yake ambavyo unaitaji utafsiri kwanza ndio utaweza kupata ujumbe ndani yake.
2: Kuna Ndoto ambazo zilizobeba vitu ndani yake ambayo maana yake ipo wazi havihitaji tafsiri ili kupata ujumbe wake.
Mathayo 1:18-24
✅Kuna ndoto nyingine haziitaji tafsisi vitu vilivyo ndani yake vipo wazi kabisa na ujumbe upo wazi
3: Kuna ndoto nyinge ambazo zina ujumbe peke yake hazijabeba vitu vingine zaidi ya ujumbe.
Mathayo 2:12,22
✅Kuna Doto zipo tofauti tofauti lazima uombe Mungu akusaidie katika kuzielewa.
2⃣: Omba Mungu akupe kufaham ujumbe wa ndoto, usiishie kufaham tafsiri yake peke yake.
Daniel 4:4-19,27
✅Ulicho kiona ndani ya ndoto ni kibaya lakin kinaweza kugeuzwa.
✅Usiishie tuu kutafuta tafsiri ya hiyo ndoto na kujua maana yake ila ombea kujua maana ya ujumbe uliobebwa na hiyo Ndoto.
3⃣: Usipofanya Maombi ipasavyo ili ujue namna ya kushugurikia ujumbe wa ndoto ipasavyo, ujumbe huo unaweza kugeuka kuwa jaribu kwako.
✅Kama umeota watu wamevaa nguo nyeupe na wewe unawafata ila wao wanakukimbia basi jua ya kuwa Muda wako wa kufa umefika au umekaribia na Mungu anataka utengeneze ukiwa duniani (uokoke) kabla ya muda wako haujafika. Maana vazi jeupe ni vazi la wokovu.
💎KWA NINI MUHIMU KUFATILIA UJUMBE WA NDOTO💎
🔅Ni kwa sababu ndani ya ujumbe uliomo ndani ya ndoto kuna taarifa ndani yake ili kukuandaa au kukuepusha na yaliopo mbele yako.
💠Mfano kutoka ktk Biblia kwa Yusufu mwana wa Yakobo.
Maisha ya Yusufu yalijengwa ndani ya ndoto saba nakati ya hizo ndoto mbili aliota yeye, nne alitafsiri na moja ilikuwa inajieleza yenyewe.
✅Ndoto ya kwanza na ya pili aliota mwenyewe.
Mwanzo 37:5-11
✅Ndoto ya tatu mnyweshaji wa Faraho aliyekuwa gerezani.
✅Ndoto ya ya nne ni ya mwokaji mikate wa Faraho aliyekuwa gerezani.
✅Ndoto ya mbili zilizo fatta aliota faraho kwa usiku mmoja..
Mwanzo 41,45
✅Ndoto ya saba ni ya baba yake Yusufu ambaye ni Yakobo.
Mwanzo 46:1-5
♻Linganisha na Zaburi 105:17-21
🔴KUMBUKA.. Usipojua kuombea ipasavyo ujumbe uliopo dani ya ndoto ahadi inageuka jaribu.
🔺Ujumbe uliopo ndani ya ndoto iliyo toka kwa Mungu ni neno lake Mungu kwako.
✅Kuna ndoto ambazo Mungu atakupa, na ujumbe wake unaweza ukawa na maagizo ya kuweza kusubiri kwa muda mrefu ili hiyo ndoto iweze kutimia.
✔Kuna wakati ambapo watu wanakufanyia fujo ktk maisha yako ila sio tuu kwa sababu wanakuchukia ila ni kwa sababu wanawinda ndoto yako isije timia katika maisha yako.
✔Sio kila ndoto utatakayo ota unatakiwa kuwaambia ndugu zako au watu maana hao wanaweza kuwa adui kwako na wanaweza kukukasirikia, bali kuwa unaliombe tu.
✔Ndoto ambayo Mungu atakuotesha katika maisha yako lazima tuu itimie juu ya Maisha yako haijalishi unapitia magumu kiasi gani.
✔Hautakiwi kuwa na kinyongo juu ya ndugu zako au wale wanaokuchukia kwa kuota kwako.
✔Hautakiwi kumkasirikia Mungu wako pale unapokuwa unasubiri ndoto yako kutimia.
✔Kama wewe ni mwana wa Mungu na umepitia mateso mengi na majaribu unaweza kumwomba Mungu akayafipisha hayo mateso yako, wewe mtegemee Mungu.
✳VITU AMBAVYO VINAWEZA KUKUSAIDIA KUSUBIRI NDOTO YAKO
1⃣ Hakikisha ndani ya ndoto umepata Ujumbe (neno la Bwana lililopo ndani yake).
✔Maana yake utalipata kwa kutafuta ujumbe hutalipata kwa kutafuta tafsiri peke yake.
2⃣ Uhusiano wako na Mungu uchukuwe nafasi ya kwanza katika Maisha yako.
✔Kuwa na Neno la Mungu ndani yako maanalitakuwa ni chakula cha kukusaidia pale utakapo pitia mahali pagumu katika maisha yako.
✔Unapopata neno la Bwana na ukalichukua kuwa lako binafsi hilo neno linageuka kukuandaa kwa ajili ya maisha yako ya baada na kuwa nuru , uponyaji juu ya maisha yako.
✔Unapo anza kuomba juu ya ndoto zako mwombe Mungu akupe tafsiri ya neno kutoka kwenye Biblia kwa maana hakuna ndoto utakayo ota isiwe na tafsiri yake hata kama iyo ndoto imetoka kwa shetani.
3⃣: Uhusiano wako na watu wanaokuzunguka.
✔Kama Mungu amekubebesha kitu katika maisha yako huitaji kugombana na watu kwa maana nafasi ambayo Mungu amekuandalia ni ya muhimu sana kuliko kugombana na watu.
4⃣: Nguvu za Mungu zitakazo kawa juu yako
Mithali 24:10
✔Ukisikia kuchoka au kukata tamaa siku ya jaribu au taabu wakati unasubiri wakati wa Bwana basi jua Nguvu zako ni chache. Nguvu ni Roho Mtakatifu ndani yako.
✔Unapokuwa upo kwenye jaribu unatumia Nguvu nyingi sana ndani yako hivyo unatakiwa uhakikishe unapata nguvu mpya. USIKATE TAMAA
Usikate tamaa maana wewe unaweza kuwakatisha au kuwasimamisha watu wengine wanao kuzunguka.
💎Mwl alifanya maombi kwa wale walio kata tamaa ili Nguvu za Mungu zishuke ndani yao kwa upya.
SHARE NA WENGINE WAKUWE KIROHO
Mungu akubariki sana
✳❇ Siku ya Nne ✳❇
💫🌱🙏🏻✨💧💐🌷🌴💫🌱🙏🏻✨💧💐🌷🌴💫🌱🙏🏻✨
There is greatness inside of you
I believe that there is a seed of greatness in all human beings. Therefore the aim of my blog is to bring to my readers awareness of things that are happening around us. I will focus majorly on inspirational news that can motivate my readers to doing more with their lives too. If you are too busy to get acquainted with what is in the newspapers or you have read the papers but have not felt any inspiration or motivation, please log on this page and be inspired to walk in your purpose and dream.