Thursday, February 23, 2017
MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017
- Next You are viewing Most Recent Post
- Previous Denice Simeo Youth Development Expert atoa ushauri kwa vijana wa chuo
google+
There is greatness inside of you
I believe that there is a seed of greatness in all human beings. Therefore the aim of my blog is to bring to my readers awareness of things that are happening around us. I will focus majorly on inspirational news that can motivate my readers to doing more with their lives too. If you are too busy to get acquainted with what is in the newspapers or you have read the papers but have not felt any inspiration or motivation, please log on this page and be inspired to walk in your purpose and dream.
💫💐✨🌴🌱🌷💫💐✨🌴🌱🌷💫💐✨🌴🌱🌷💫💐✨🌴🌱🌷💫💐✨🌴🌱🌷
*SEMINA YA NENO LA MUNGU MBEYA MJINI*
*Mwl. C. MWAKASEGE*
SOMO: *NAMNA YA KUOMBEA NDOTO ZILIZOGUSA MAISHA YAKO*
DAY 1
💧💧💧💧💧💧💧💧💧💧
LENGO; *KUIMARISHA UHUSIANO WAKO NA MUNGU KATIKA YESU KRISTO.*
➡Ni mara chache sana kujifunza somo la namna hii na halionyeshi kama lina umuhimu sana kwa watoto wa Mungu kwahiyo watu hawalipi muitikio mkubwa sana. LAKINI ni muhimu sana Kujifunza na Mungu anatamani tupate kujifunza.
🔹Ni somo linalozaa matunda makubwa sana.
NOTE: *Ni vigumu sana kuuliza ndoto ya Mungu kwa shetani....Fumbo la Mungu lina fumbuliwa na Mungu mwenyewe.*
JAMBO LA KWANZA:
*USIIDHARAU AU USIIPUZIE NDOTO ULIYOOTA HII NI KWASABABU NDOTO NI LANGO MOJA WAPO LA KIROHO AMBALO MUNGU NA SHETANI WANALITUMIA KUMFIKIA MWANADAMU.*
-Kati ya ulimwengu wa roho na ulimwengu wa mwili kuna ukuta.na dhambi ilipoingia ilitengeneza ukuta mwingine kwahiyo Mungu alitengeneza malango ambayo yatasaidia mawasiliano kati ya ulimwengu wa roho na ulimwengu wa mwili.
Mfano wa malango hayo;
1. *Muda ni lango,*
2. *Ndoto ni lango.*
*MIFANO JUU YA LANGO LA NDOTO;*
MFANO WA KWANZA
🔹Mwanzo 41:1-7,8 (Ndoto ya farao)
-Ndoto si ndoto tu ina ujumbe ndani yake.
-kama ndoto ya farao isingebeba roho ya kumfadhaisha angeipuuzia na asingeifuatilia.
NINI KINGETOKEA.-kungekua na miaka saba ya Mafanikio na miaka saba ya mahangaiko.
➡Mwanzo41;53-57
🔹Dunia nzima ingepata shida kwa ajili ya farao kama angepuuzia ile ndoto na huenda watu wangemlaumu Mungu kwakuto kusema nao juu ya njaa.
MFANO WA PILI;
🔹Ayubu 33;14-19
Ndoto inapokuja haiji tu pia inakuzibua masikio yako ya ndani.
-Ndoto inaachilia ufahamu juu ya mambo *yaliyopita, yaliyopo na yajayo.*
-Mungu anaweza kutumia ndoto kufikia nafsi ya mtu,mwili wa mtu na kupangua makusudio yasiyo yake.
MFANO WA TATU.
🔹Kumbukumbu 13;1-4 Hesabu 12:6
-Mungu anatumia ndoto na shetani anatumia ndoto...
Aliyetengeneza Ndoto ni Mungu lakini shetani anatabia ya kuiga malango ya Mungu lakini hanauwezo wa kuyatengeneza malango hayo ila dhambi ndo inayompa ruhusa ibilisi kumiliki malango ambayo Mungu anatamani tuyamiliki.
-Ukipuuzia ndoto kunagharama kubwa sana iwe ndoto toka kwa Mungu au ndoto za shetani usipojua namna ya kufanyia kazi gharama yake ni kubwa.
➡KWAHIYO;
🔸Jambo unaloota linaweza kujitokeza katika nafsi yako,roho yako na mwili.
🔸Jambo unaloota likiwa na maelekezo na ukayafuata matokeo yake yataonekana katika maisha yako yawe mazuri au mabaya.
*MTU ANAPOOTA NDOTO ANAKULA CHAKULA NA WATU WALIOKUFA AU ASIOWAJUA.*
(1Wakorintho10:15-22).
-1) Chakula kwenye ndoto inawezekana kabisa ni ushirika wa kiagano kati ya muotaji na hao aliowaota kwenye ndoto wakiunganishwa na roho iliyoleta iyo ndoto na madhabau iliyobeba ndoto iyo na ushirika huo utajitokeza katika mwili Lakini pia matokeo yatatokea kwenye sadaka.
➡ndiomaana eneo lolote lenye tatizo kama hilo ni vigumu sana kumtolea Mungu...sadaka zao zimebanwa kwenye maagano na wanazuiwa kumtolea Mungu aliyehai.
2) Hali ya kiroho ya muotaji inabadilika.
-mzigo wa kumtumikia Mungu unakufa,Kiu ya kuomba inapotea.
3) Inawezekana pia huna agano popote lakini ndoto iyo inaashiria kuna agano jipya linataka kufungwa kwako.
NOTE:-
*Agano linaweza kufungwa kwa ndoto..Ibrahimu alifunga agano na Mungu kwandoto* *Mwanzo 15:1-20*
4). Ndoto kama hiyo inaweza ikawa imekuja kukujulisha kua umefika muda au wakati wa kuingia kwenye agano au utumishi husika mfano petro *(matendo 10:1-11).*
-Ndoto zinamaana yake kwenye Biblia pia kumbuka sio kila wakati waliokufa wanapokujia inamaanisha ni ndoto ya kipepo...Ndiomana unahitaji kujua maana yake.
-Maswala ya ndoto si ndoto tu ni masuala halisi.
*MUNGU AKUBARIKI USIKOSE DAY 2*
💫💐✨🌴🌷🌱💧💫💐✨🌴🌷🌱💧💫💐✨🌴🌷🌱💧💫💐✨🌴🌷🌱💧💫💐
There is greatness inside of you
I believe that there is a seed of greatness in all human beings. Therefore the aim of my blog is to bring to my readers awareness of things that are happening around us. I will focus majorly on inspirational news that can motivate my readers to doing more with their lives too. If you are too busy to get acquainted with what is in the newspapers or you have read the papers but have not felt any inspiration or motivation, please log on this page and be inspired to walk in your purpose and dream.