MAKOSA AMBAYO YANAWEZA KUFANYA MMILIKI WA BUS KUFUNGIWA KUTOA HUDUMA | Apostle Darmacy Blog MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 | Apostle Darmacy Blog

APOSTLE DAMAS

Breaking News

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, February 23, 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 

 

Goo

 

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 
About Muses Radio Player...
Version 2.1 (html5)

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.
-->

Tangaza nasi

Breaking News
Loading...

Soma App

Soma App
DOWNLOAD Somaapp NOW!

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, August 18, 2016

MAKOSA AMBAYO YANAWEZA KUFANYA MMILIKI WA BUS KUFUNGIWA KUTOA HUDUMA

MAKOSA AMBAYO YANAWEZA KUFANYA MMILIKI WA BUS KUFUNGIWA KUTOA HUDUMA

Mmiliki wa bus la abiria au mwendeshaji wa huduma hiyo, anaweza kufungiwa kutoa huduma na mamlaka iwapo atashindwa kuzingatia mojawapo kati ya haya yafuatayo:
1. Kutozingatia kanuni za kiusalama za abiria, kama vile
(a) Kutofanya matengenezo ya mara kwa mara ya magari yake kiasi cha kufanya magari hayo kuwa hatari kwa usalama wa abiria au kuharibika haribika hovyo njiani;
(b) Gari kutokidhi viwango vya kuwepo barabarani, yaani roadworthiness
(c) Kujenga bodi juu ya chesisi ya lori
(d) Endapo fremu ya chesisi, ekseli,springi, na rim zimeungwa ungwa kwa welding
(e) Ujenzi wa bodi kutozingatia viwango vya TBS
(f) Uchakavu wa gari, mfano Sakafu ya gari kuwa yenye utelezi, na iliyochubuka na yenye isiyolinda abiria dhidi ya vumbi, unyevu, hewa chafu, shoti za umeme, na kelele.
(g) Gari kujaza mafuta au kufanya matengenezo huku likiwa na abiria
(h) Kuhatarisha usalama wa abiria kwa kuacha mlango wazi wakati gari linatembea au wakati wa kuondoka
2. Kutowasimamia vema kondakta na dereva kuzingatia kanuni za usalama na ubora wa huduma pamoja na masharti mengine ya usafirishaji.
3. Kutozingatia ubora wa huduma kwa abiria, mfano abiria kutopata huduma kulingana na fedha waliyoilipia; kutozingatia usafi, kutotoa huduma kwa abiria baada ya bus kuharibika au kutekeleza abiria
4. Gari kutokuwa na bima
5. Kutozingatia masharti ya leseni ya usafirishaji ambayo ni
(a) Kuhakikisha wafanyakazi wake wakiwa kazini hawafanyi mambo yafuatayo yaliyokatazwa:
(i) matumizi ya lugha mbovu na za uhasama;
(ii) kuzuia au kufanyia fujo magari mengine;
(iii) kuendesha kwa mwendo kasi Zaidi ya ule uliowekwa kisheria na kufanya mashindano ya kugombania abiria;
(iv) kukatisha ruti kabla ya kufika mwisho wa safari
(v) kuendesha wakiwa wamelewa
(vi) kuendesha kwa hatari na kwa kupuuzia hatari au kinyume cha sheria ya usalama barabarani
(vii) kuwakatili abiria
(viii) kuwazuia au kuwakatili wanafunzi;
(ix) kuendesha huku wakitumia simu;
(x) kupakia wanyama na vitu vya hatari kwenye gari.
(b) Kuzingatia ruti na ratiba (kif.19(1))
(c) Kuripoti kwa mamlaka ikiwa gari lake halitatoa huduma kwa siku thelathini na Zaidi au kama halitaweza kufanya safari kwa masaa 24 yajayo
(d) Kutoa usafiri kwa abiria kulingana na masharti na vigezo vilivyopo kwenye tiketi, ratiba na kutoa usafiri mbadala wa hadhi ile ile inapotokea gari husika limeharibika.
(e) Kuondoa gari barabarani mara moja baada ya kuharibika, na pia kufanya marekebisho ya gari ndani ya masaa mawili tangu lilipoharibika.
(f) Ikiwa gari halitatengemaa ndani ya masaa mawili basi mmiliki atatakiwa kuwatafutia abiria usafiri mbadala au kuwarudishia nauli kamili. [kif.22(1)na(2)]
(g) Kutochaji mzigo usiozidi kilo 20 [kif.23(1)]
(h) Kutoa tiketi
6. Kutorekebisha makosa au mapungufu mbalimbali yanatojitokeza katika uendeshaji wa biashara yake hata baada ya kuwa ameshaarifiwa au kuonywa na SUMATRA.
NB: Mambo yaliyoanishwa hapo juu yatafanya mmiliki afungiwe kutoa huduma iwapo tu yamejitokeza mara kwa mara au hata kama ni mara moja yamekuwa katika kiwango ambacho hakikubaliki au kuvumilika kuruhusu kampuni au gari husika kuendelea kusafirisha abiria, mathalani pale ambapo gari litakutwa halina mikanda, tairi zote kipara, halina bima na sehemu ambazo hazitakiwi kufanyiwa welding zimefanyiwa welding. Hapa mamlaka inaweza kusimamisha huduma husika mara moja ili gari husika lifanyiwe marekebisho.

Kwa ufupi hizo ndizo sababu zinazoweza kupelekea mtoa huduma kufungiwa kutoa huduma.
Ni Imani yangu sasa utakuwa umepata uelewa angalau wa vigezo gani vinatumika kufungia kampuni kutoa huduma. Kwa maelezo Zaidi maafisa wa SUMATRA wataongezea ufafanuzi.
RSA TANZANIA
USALAMA BARABARANI NI JUKUMU LETU SOTE.
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.