REDIO USHINDI YAWEKWA WAKFU, WACHUNGAJI WATAKIWA KUITUMIA KUENEZA INJILI. | Apostle Darmacy Blog MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 | Apostle Darmacy Blog

APOSTLE DAMAS

Breaking News

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, February 23, 2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017

MAGAZETI YA LEO IJUMAA FEBRUARY 24,2017 

 

Goo

 

Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 
About Muses Radio Player...
Version 2.1 (html5)

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.
-->

Tangaza nasi

Breaking News
Loading...

Soma App

Soma App
DOWNLOAD Somaapp NOW!

Gospel Awards

Gospel Awards
GOSPO AWARDS ni tuzo maalum zilizoanzishwa na kampuni ya Gospo Media kwa waimbaji, wanamuziki, na wataarishaji wa muziki wa Injili walioweza kufanya vizuri kupitia tovuti ya gospomedia.com, mitandao ya kijamii, radio na tv kwa mwaka 2016 kutoka Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla.

RSA TANZANIA

RSA TANZANIA
RSA ni kifupi cha maneno ROAD SAFETY AMBASSADORS ikiwa na maana Mabalozi wa Usalama Barabarani.

Radio Sayuni

ASAS Dairies LTD

Soma BIBILIA

Soma BIBILIA

Thursday, July 10, 2014

REDIO USHINDI YAWEKWA WAKFU, WACHUNGAJI WATAKIWA KUITUMIA KUENEZA INJILI.

NI KATIKA  KUELEKEA MAHADHIMISHO YA MIAKA 75  YA KANISA LA T.A.G

 Makamu askofu  Dk. Magnus Mhiche. wa T.A.G akikata utepe kuzindua na kuweka wakfu kituo cha Redio Ushindi kwaniaba ya askofu mkuu wa kanisa la T.A.G Dk. Barnabas Mtokambali
Wachungaji na wageni waalikwa wakikiombea kituo hicho
 Makamu askofu  Dk. Magnus Mhiche. wa T.A.G akipata maelezo mafupi toka kwa watangazaji wakituo hicho mara tu baada ya uzinduzi
 Makamu askofu  Dk. Magnus Mhiche. wa T.A.G  akiongea na wageni waalikwa wakati wa uzinduzi wa kituo cha Redio ushindi
ASKOFU wa TAG Jimbo la Mbeya Kaskazini, Dk. Donald Mwanjoka akisalimia wageni waalikwa katika uzinduzi huo
Meneja wa Redio hiyo, Mathew Sasali, akisoma taarifa fupi ya kituo hicho
Kwaya Mbali mbali zilitumbuiza katika uzinduzi huo
Baadhi ya wageni waalikwa wakifuatilia matukio ya uzinduzi kwa makini
Baadhi ya wafanyakazi na watangazaji wa kituo cha Redio Ushindi
Mhariri Mkuu wa Redio Ushindi, Robin Ulikaye akisoma risala





ASKOFU mkuu wa Kanisa la Assemblies Of God Tanzania (TAG) Dk. Barnabas Mtokambali, amewataka waumini na watumishi wa kanisa hilo kutumia kituo cha Redio Ushindi kueneza injili.
Kauli hiyo ilitolewa jana wakati wa kuwekwa Wakfu kwa kituo cha Redio cha Ushindi kinachomilikiwa na TAG kilichopo Isyesye Jiji na Mkoa wa katika hafla iliyofanyika katika Studio za redio hiyo ambapo Askofu huyo aliwakilishwa na Makamu wake Dk. Magnus Mhiche.  
Akizungumza kwa niaba ya Askofu Mkuu, Dk. Mhiche alisema kituo cha REDIO Ushindi ni kama chombo ambacho wachungaji wanaweza kukitumia kuvuna waumini na kueneza injili kirahisi kuliko kutembea kwa mguu kuwafuata waumini.
Alisema redio huwafikia watu wengi zaidi bila kujali mazingira walipo hivyo ni kama kanisa linalotembea ambalo linaweza kusaidia harakati na mkakati wa kanisa wa kuwavuta waumini wengi hatimaye kuongeza idadi ya wafuasi wa kanisa la TAG tofauti na ilivyo sasa.
Aidha aliwataka wafanyabiashara na watu mbali mbali kutumia kituo hicho kutoa matangazo ya biashara zao pamoja na huduma ili kuendelea kuunga mkono huduma zinazotolewa na redio hiyo ili iweze kujiendesha na kuendelea kuwepo.
Hata hivyo Askofu huyo aliwaagiza wasimamizi wa Redio hiyo kutopokea matangazo yasiyokuwa na maadili ya kidini kwa madai ya kujali fedha kuliko kuangalia maudhui ya tangazo lenyewe kama linakiuka miiko ya kanisa.
“ Nitumie nafasi hii kuwaagiza wasimamizi wa redio sio kila tangazo linatakiwa kupokelewa hapa angalieni maadili matangazo ya madawa ya kienyeji au pombe hayatakiwi ni bora tukakosa fedha kabisa” alisisitiza Askofu huyo.
Kwa upande wake Meneja wa Redio hiyo, Mathew Sasali, alisema kituo hicho kilifunguliwa Juni 1, 2011 hivyo hadi kuwekwa wakfu kinatimiza miaka 3 na sherehe hizo ni sambamba na maadhimisho ya miaka 75 tangu kuanzishwa kwa kanisa la TAG nchini Tanzania.
Aidha katika Risala ya Kituo hicho iliyosomwa na Mhariri Mkuu wa Redio Ushindi, Robin Ulikaye, ilisema baadhi ya mafanikio waliyoyapata ni pamoja na kuongeza idadi ya wasikilizaji, kueneza injili kupitia Redio pamoja na kuongezeka kwa idadi ya watumishi kutoka 6 hadi 13 sasa.

  Source;  Mbeya yetu
JOSEPH MWAISANGO
MWANDISHI MKUU
j.mwaisango@tonemg.com
+255 754 374408
Toa Maoni Hapa Chini

google+

linkedin

 

NURU MINISTRY

PURE MISSION

PURE MISSION
MAPINDUZI YA FIKRA

Apostle Damasy

Apostle Damasy

Emare Arts Collection - E.A.C

Emare Arts Collection - E.A.C
Sw: Karibuni kwa ununuzi wa picha za kitamaduni ili kukuza Sanaa ya nyumbani, kupitia 0625 927 752 au 0758 576 065, Bei ni nzuri, Asanteni! ******* Eng: Welcome for purchasing different Africultural Arts, as to boost the market of African cultural products via the numbers 0652 927 752 or 0758 576 065. The prices are affordable, Thank you!

ABC Studio Mwanza

ABC Studio Mwanza
Photograph,Video shooting & all Printing works +255756143999, +255658720091, We are located at New Post Office Pamba Road & Nyerere Road, Mza Tz www.facebook.com/abcmwanza,www.youtube.com/abcstudiomwanza
apostledarmasy. Powered by Blogger.